• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TASAF kuzifikia kaya masikini zaidi ya milioni 1.4 nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: February 25th, 2021

AWAMU ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) inatarajia kuzifikia kaya masikini zaidi ya milioni 1.4 zinazokadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni saba kote nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga wakati anafungua mafunzo ya siku sita ya timu maalum ya wawezeshaji 25 kutoka Halmashauri za Madaba na Songea wilayani Songea yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Ushirika mjini Songea.

Mwamanga amesema wawezeshaji hao watahusika na utekelezaji na usimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF Awamu ya tatu katika kipindi cha pili.

“Miradi ya kutoa ajira za muda inalenga kutoa ajira kwa kaya masikini wakati wa kipindi cha hari ili wanakaya hao wasiweze kuuza rasilimali walizonazo kwa ajili ya kupata fedha na kuwezesha ajira kwa kaya ili kuongeza kipato hivyo kupunguza umaskini’’,alisema.

Hata hivyo amezitaja kaya zitakazoshiriki utekelezaji wa miradi hiyo ni zenye watu wenye uwezo wa kufanya kazi na wenye umri wa kuanzia miaka 18 hadi 65.

Mwamanga amesema  katika kipindi cha kwanza cha mpango wa kunusuru kaya masikini jumla ya miradi 9,440 ya kutoa ajira za muda ilitekelezwa  kwa gharama ya shilingi bilioni 1.19 kati ya hizo shilingi bilioni 83.3 zilitumika kwa kulipa ujira wa walengwa na shilingi bilioni 35.7 kwa ajili ya vifaa vya miradi na usimamizi.

Kwa upande wake Mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka TASAF Makao Makuu Frank Antony  amelitaja lengo la mafunzo hayo kuwa ni kujenga uwezo wa timu za watalam ngazi ya Halmashauri za Songea na Madaba kuhusiana na uibuaji,uandaaji,utekelezaji na usimamizi miradi ya kutoa ajira za muda kwa walengwa ngazi ya jamii.

Amesema mafunzo hayo ya nadharia na vitendo ya siku sita ambayo yametolewa kwa wawezeshaji 25 toka Halmashauri mbili za Madaba na Songea yatawapelekea maarifa jumla ya walengwa wa TASAF 5,400 kati yao walengwa 3,800 toka Halmashauri ya Songea na walengwa 1,600 toka Madaba.

“Baada ya mafunzo haya tunategemea  wawezeshaji watakwenda kuwasaidia walengwa ngazi ya jamii kuibua miradi ngazi ya jamii yenye tija na itakayoonesha thamani ya fedha’’,alisisitiza Antony.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Athuman Nyange ameitaja miradi iliyotekelezwa katika kipindi kilichopita kuwa ni uboreshaji wa visima vya asili,ujenzi wa vivuko vya watembea kwa miguu,uchimbaji mabwawa ya samaki na uanzishwaji vitalu vya miche ya miti.

Nyange ametoa rai kwa wawezeshaji,baada ya mafunzo kuibua miradi yenye tija na yenye kuonesha thamani ya miradi kwa awamu ya pili.

Naye Vitalis Jarando Mwezeshaji aliyepata mafunzo hayo toka Halmashauri ya Wilaya ya Songea amesema mafunzo hayo yatawawezesha kutoa mafunzo ngazi ya jamii na kuleta tija kwa jamii.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 24,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.