• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TASAF Songea kujenga nyumba ya Mganga

Imewekwa kuanzia tarehe: October 25th, 2022

MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya Songea mkoani Ruvuma Menas Komba,amewakumbusha watumishi wa Halmashauri hiyo  suala la uaminifu na uadilifu wanapopewa dhamana ya kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo ili kuepuka miradi  kujengwa chini ya viwango.

Komba ametoa rai hiyo jana,wakati akizungumza na wananchi na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo wakati akabidhi eneo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mganga wa Hospitali ya wilaya katika kijiji cha Mpitimbi B wilayani Songea.

“hatuhitaji ubabaishaji katika mradi huu,tumepata shida sana kwenye baadhi ya miradi iliyotekelezwa uko nyuma,kuna mama mmoja alipewa kazi ya kusimamia miradi katika maeneo tofauti, sasa alichotufanyia hatuwezi kumsahau hata kidogo”.

Aidha,amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Neema Maghembe na wakuu wa idara kuhakikisha wanawapa kazi  watu(mafundi) wenye uwezo  ambao watafanya kazi kwa viwango kulingana na gharama halisi ya fedha zinazotolewa na Serikali.

“mkurugenzi sisi katika Halmashauri tuna mafunzi wazuri sana,waombe watatu au zaidi na washindanishwe ili apatikane mmoja mwenye uwezo kwa kufuata utaratibu na siyo kuteuliwa”alisisitiza Komba.

Komba,amewaasa wataalam wa Halmashauri hiyo kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa  katika maeneo mbalimbali yenye lengo la kuboresha  huduma za kijamii na maisha ya wananchi na kuacha tabia ya kutanguliza maslahi  binafsi  kwa kuwa tabia hiyo inasababisha matumizi mabaya ya fedha za umma na kuwepo kwa miradi mibovu.

“msinunue vitu ambavyo viko chini ya viwango alafu vikatusumbua,pia mjiepushe kuongeze gharama ya bei  kwenye manunuzi ya vifaa,tutakapogundua tutafuta hiyo kotesheni na kuchukua hatua za kinidhamu kwa mtumishi aliyehusika”aliongeza.

Mwenyekiti huyo wa Halmashauri,amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia mpango wa Tasaf kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kaya maskini hapa nchini  na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama,kwa kutafuta fedha kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi wa Jimbo hilo.

Alisema,nyumba hiyo itakwenda kupunguza tatizo la nyumba za watumishi na kusogeza huduma za afya  karibu na wananchi kwani nyumba hiyo itamwezesha Daktari kuishi jirani na eneo la kazi.

Komba ambaye ni Diwani wa kata ya Matimila,amewataka wasimamia wa mradi huo kuwa na daftari lenye orodha ya wanufaika wote watakao shiriki katika ujenzi wa nyumba hiyo ili siku ya malipo kusitokee malalamiko yasiokuwa  ya lazima.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Neema Maghembe alisema,shilingi milioni 68  zilizoletwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo zitatumika vizuri kama ilivyopangwa.

Alisema,Halmashauri kupitia wataalam wa  idara imejipanga kuhakikisha miradi yote inayotekeleza na ile itakayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ikiwamo ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa inakamilika kwa muda uliopangwa.

Kwa upande wake katibu tawala wa wilaya ya Songea Pendo Daniel,ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuunga mkono mapambano dhidi ya umaskini kwa kutoa ruzuku ya fedha  kwa wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini hapa nchini.

Amewataka wananchi wa kijiji hicho ambao ni walengwa wa mpango huo ,kujitokeza na kushiriki  kwa karibu ujenzi wa nyumba hiyo ili  waweze kujipatia kipato na ikamilike kwa muda uliopangwa.

Aidha,amewaagiza wasimamizi kutoa vifaa vya ujenzi kwa wakati ili mafundi waweze kutekeleza majukumu yao na kuweka maslahi ya Taifa mbele badala ya kutanguliza maslahi yao binafsi.

Awali Mtendaji wa kijiji cha Mpitimbi B Naomi Julius alisema,fedha zinazotarajiwa kutumika katika mradi huo ni Sh,milioni 68,376,000.0 zilizookolewa katika manunuzi ya vifaa vya miradi ya ajira za muda kwa mwaka 2021/2022.

Alisema, kwa kuwa fedha za kugharamia ujenzi wa nyumba ya Mganga zinatokana na utekelezaji wa miradi ya ajira za muda,ujenzi wa nyumba hiyo utafanywa na wana kaya wenye uwezo wa kufanya kazi toka kaya za walengwa wa kijiji hicho.

Alisema,muda wa utekelezaji wa mradi huo ni miezi sita na walengwa watafanya kazi kwa siku kumi kila mwezi na kila mlengwa atalipwa sh.3,00 kwa siku  ili kuwawezesha kupata ruzuku au kipato cha ziada kwa ajili ya kujikimu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.