• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TEMBO wavamia mashamba Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: July 19th, 2023

KUNDI kubwa la Tembo wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 20, wamevamia katika makazi ya watu na mashamba katika kijiji cha Majimaji wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,na kufanya uharibifu na kula mazao mbalimbali.

Tembo hao wamesababisha hasara kwa wananchi wa kijiji hicho  akiwemo Iman Kalembo,ambaye amepoteza mazao yake baada ya shamba lake lililokuwa na mapapai na miembe lenye ukubwa wa ekari 4 kuvamiwa na wanyama hao.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa Kalembo alisema,Tembo wamekula mapapai ambayo yalishaanza kukomaa na mengine kuanza kuiva,lakini ndoto zake za kujikwamua na umaskini kupitia kilimo zimeyeyuko kutokana na  uvamizi  uliofanywa na wanyama hao.

Kalembo,ameiomba Serikali kuchukua hatua za kudhibiti tembo hao wanaozurura ovyo kwenye makazi ya watu na mashambani na kula mazao,hali inayotishia kuwepo kwa upungufu  mkubwa wa chakula  katika kijiji hicho.

Msimamizi wa shamba hilo Ramadhan Kaundama alieleza kuwa,kundi la tembo lilianza kufika katika maeneo hayo saa 11 jioni lakini wananchi walifanikiwa kuwafukuza,hata hivyo usiku Tembo walirudi tena na kula mazao na kufanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ya shamba hilo na mashamba ya wakulima wengine.

Aidha alisema,sasa wananchi wanashindwa kwenda mashambani  kwa kuhofia kuvamiwa na tembo na baadhi yao wanalazimika kutoa mazao mashambani yakiwa hayajakomaa kwa kuhofia kuliwa.

Mkulima mwingine Sophia Imani amelalamikia uvamizi wa tembo kwenye mashamba na makazi yao,hali inayozidi kuhatarisha usalama wao na mali zao.

Alisema,licha ya kutoa taarifa kwenye mamlaka zinazohusika,lakini bado tembo wamezidi kuongezeka na kuendelea kuvamia kwenye shamba lake mara kwa mara.

Aliongeza kuwa, kuwepo kwa makundi  ya tembo wanaofika hadi maeneo ya makazi yao usiku na mchana wanasababisha hata wanafunzi kushindwa kwenda shuleni na wengine kuchelewa vipindi vya asubuhi kwa kuhofia usalama wao.

Kwa upande wake Afisa Wanyama pori  wilayani Tunduru Dauson Francis alisema,kimsingi wilaya ya Tunduru imeanzishwa na kuzungukwa katika maeneo ya mapito ya wanyama hasa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere zamani Selou.

Alisema,kuongezeko la matukio ya  migogoro baina ya tembo na binadamu linachangiwa na mambo mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa shughuli kibinadamu katika maeneo ya mapito ya wanyamapori na yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi.

Alitaja changamoto nyingine ni ongezeko la watu na vijiji kutokuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi,hivyo kusababisha wananchi kupewa ardhi  kwa ajili ya kulima na kufanya shughuli nyingine za kibinadamu kwenye mapito ya wanyamapori.

Alisema,chanzo kingine cha migogoro ni uingizwaji wa mifugo katika maeneo yaliyohifadhiwa na hivyo kusababisha tembo kutoka hifadhini kwani baadhi ya mifugo huwa na harufu za dawa za kuzuia magonjwa jambo ambalo tembo hawapendi.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.