• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TFS TUNDURU yatoa msaada wa vifaa vya ujenzi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 16th, 2022

WAKALA wa huduma za misitu Tanzania(TFS)wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,imetoa msaada ya vifaa mbalimbali vya ujenzi kwa ajili ya ukarabati wa zahanati ya kijiji cha Misechela wilayani Tunduru.

Msaada uliotolewa na TFS ni mifuko 60 ya saruji,bati 10, misumari ya bati kilo 20,rangi ya mafuta lita 40 na  rangi ya maji lita 80 vyote  vikiwa  na thamani ya Sh.milioni 2.

Akikabidhi msaada huo kwa serikali ya kijiji  hicho,Mhifadhi wa misitu (TFS) Wilayani Tunduru Denis Mwangama alisema,wakala wa huduma za misitu Tanzania kwa kuendeleza ujirani mwema na ushirikkiano wa uhifadhi wa misitu inashiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya wananchi katika vijiji vinavyopakana na misitu za hifadhi.

Alisema,kijiji cha Misechela ni miongoni mwa vijiji 13 vinavyopakana na Hifadhi ya mazingira asilia Mwambesi yenye rasilimali nyingi ikiwamo wanyama aina mbalimbali,miti na mto maarufu wa Ruvuma unaopita katika wilaya zote tano za mkoa wa Ruvuma na baadhi ya wilaya za mkoa wa Mtwara.

Alieleza kuwa,kwa kutambua umuhimu wa afya ofisi ya wakala wa huduma za misitu Tanzania wilaya ya Tunduru inaungana na wananchi wa kijiji cha Misechela katika kazi ya ukarabati wa zahanati ya kijiji hicho kwa kutoa vifaa vya ujenzi kama mchango wake.

Alisema,TFS itaendelea kushiriki na kushirikiana na jamii  katika kuboresha sekta ya afya kwa kuamini kuwa,jamii  ya watu wenye afya njema wanamchango mkubwa katika kutunza rasilimali za misitu  kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha alisema,jamii na serikali za vijiji kila upande  una wajibu wa kuhakikisha wanatunza misitu kwa kuwa,misitu ni sehemu ya chanzo kikubwa cha mapato inayoingizia Taifa fedha nyingi ambazo zinatumika kwa kuboresha na kuimarisha huduma mbalimbali za kijamii hapa nchini.

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa kijiji cha Misechela Daud Pendael, ameishukuru TFS kwa msaada huo na kuhaidi vifaa hivyo vitatumika kwa kazi iliyokusudiwa.

Alisema,kijiji cha Misechela ni miongoni mwa vijiji vyenye changamoto kubwa ya huduma za afya, hivyo wananchi wake wanalazimika kutembea umbali mrefu kwenda vijiji vingine kufuata huduma hizo.

Alisema,vifaa hivyo vinakwenda kuimarisha huduma za afya kwa kumaliza ukarabati wa zahanati ya kijiji hiyo ambayo  kazi ya ukarabati ilisimama kwa kukosa vifaa vya viwandani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.