• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TFS yatoa mizinga ya nyuki Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: June 10th, 2022

WAKALA wa huduma za misitu Tanzania(TFS)Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,imekabidhi mizinga ya nyuki kwa Serikali ya kijiji cha Mbati kwa ajili ya kuzuia wanyama waharibifu hususani Tembo wanaovamia mashamba  na kula mazao.

Akizungumza wakati wa makabidhiano  ya mizinga hiyo Meneja wa TFS Wilayani Tunduru Denis Mwangama alisema,ufugaji nyuki ni kati ya mbinu  kubwa zinazotumika na kusaidia sana kuzuia Tembo kuingia kwenye makazi ya watu na mashambani.

Alisema utafiti uliofanyika umeonesha kuwa,ufugaji nyuki umeleta mafanikio makubwa  katika  maeneo yenye changamoto ya wanyama wakali na waharibifu wanaotoka  porini au kwenye hifadhi na kwenda kwenye makazi ya watu na mashambani.

“kwa kawaida Tembo wanapopita  kwenye njia zao na kugonga mizinga au miti ambayo imefungwa mizinga hiyo,na nyuki wakipata harufu ya wanyama hao wanatoka nje na kuwang’ata  na hivyo kukimbia au kurudi wanakotoka”alisema Mwangama.

Mwangama alisema, mizinga hiyo ina thamani ya Sh.2,000,000/= na imefungwa kwenye maeneo yote ya mapito ya Tembo,kama mkakati wao wa kusaidia jamii kukabiliana na majanga mbalimbali.

Aidha alisema,TFS itaendelea kutoa mizinga kadri itakavyoweza ili kudhibiti vitendo vya uharibifu wa wanyama hao pamoja na kuhamasisha jamii kufuga nyuki kama sehemu ya kujiongezea kipato badala ya kutegemea shughuli moja tu ya kilimo.

Amewaomba wananchi wa kijiji hicho,kuhakikisha wanalinda mizinga hiyo na kuwa na utaratibu wa kukagua mara kwa mara ili kuifanyia usafi na matengenezo ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kutimiza malengo yaliyokusudiwa na Serikali.

Alisema,mizinga hiyo ni mali ya Serikali ya kijiji na sio ya mtu binafsi na ndiyo yenye mamlaka ya kutunza na kupanga matumizi yake kwa kuwashirikisha wana jamii(wananchi).

Kaimu Afisa Nyuki wa Halmashauri ya wilaya Tunduru Micheal  William,ameishukuru Wizara ya Maliasili na utalii kupitia wakala wa huduma za misitu nchini(TFS)kwa kuona umuhimu wa kutoa mizinga ya nyuki.

Alisema,mizinga hiyo itaongeza hamasa na kuongeza chachu ya ufugaji nyuki endelevu katika misitu ya asili na ile inayopandwa kama sehemu ya kipato cha mtu mmoja mmoja na jamii.

Michael alieleza kuwa,mizinga hiyo inakwenda kubadilisha ufugaji nyuki kutoka ule wa mazoea na kuwa wa kisasa na  hivyo kuwaongezea kipato chao ambapo amewataka wananchi wa kijiji hicho, kulinda na kutunza mizinga hiyo ili iweze kusaidia kukabiliana na wanyama hao.

Amewaomba wadau wengine wa sekta ya misitu na nyuki  nchini,kujitokeza na kuwasaidia wananchi wa Tunduru kukabiliana na wanyama waharibifu  wa mazao ambao wamesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi wanaotegemea shughuli za kilimo kuendesha maisha yao ya kila siku.

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Mbati Baslom Mkondya alisema, changamoto kubwa katika kijiji hicho ni Tembo ambao wanatoka kwenye hifadhi na kwenda kwenye mashamba ya wananchi  na kula mazao.

Kwa mujibu wa Mkondya ni kwamba,hadi sasa jumla ya mashamba 115 sawa na ekari 500 za mazao mbalimbali zimeharibiwa na Tembo,  jambo lililosababisha uchumi wa kijiji hicho kushuka na kutishia kuwepo kwa dalili za njaa na umaskini kwa baadhi ya kaya.

Alitaja mazao yaliyoshambuliwa na  wanyama hao ni pamoja na Mbaazi,mpunga,mahindi,korosho na matunda mbalimbali yanayolimwa kwa ajili ya kuwaongezea kipato wananchi wa kijiji hicho.

Pia alisema kuwa,wanyama hao wanatishia usalama wananchi pindi wanapokwenda katika shughuli zao za uzalishaji mali na kuiomba serikali na wadau mbalimbali kujitokeza kudhibiti wanyama  hao ili wasiendelee kuleta madhara makubwa kwa wananchi.



Mkazi wa kijiji hicho Mussa Abdala,ameishukuru TFS kupeleka mizinga hiyo kwa kuamini kwamba itasaidia sana kukabiliana na wanyama waharibifu ambao ni kero kubwa katika kijiji hicho.



Alisema,wanyama hao wamesababisha umaskini mkubwa kwa baadhi ya familia kwa kukosa chakula,kutokana na mazao yao kuliwa  yakiwa bado mashambani na kuiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti wanyama  hao wasiendelee kuleta madhara makubwa kwa jamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.