• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TRA yakabidhi gari ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 7th, 2025

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Ruvuma imekabidhi rasmi gari aina ya ISUZU kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa ajili ya matumizi ya serikali, baada ya kutaifishwa kutokana na kuingizwa nchini kinyume cha sheria.

Makabidhiano hayo yamefanyika  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea, ambapo Meneja wa TRA Mkoa wa Ruvuma, Nicodemas Mwakilembe, alikabidhi gari hilo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwakilembe alieleza kuwa gari hilo awali liliingia nchini kwa kibali cha muda mnamo Januari 2024 likitokea Kenya, lakini lilirejea tena nchini mwezi Aprili 2024 bila kufuata taratibu za kisheria.

“Gari hili lilikutwa katika Kijiji cha Lusewa, Wilaya ya Namtumbo likifanya shughuli za kubeba mizigo kuelekea Masasi, Mtwara. Jeshi la Wananchi waliopo kijijini hapo waliliona na kulikamata. Baada ya uchunguzi wa kina, ilibainika kwamba gari hilo liliingia nchini kwa njia zisizo halali,” alisema Mwakilembe.

Aliongeza kuwa baada ya hatua zote za kisheria kufuatwa, TRA iliamua kutaifisha rasmi gari hilo na kulikabidhi kwa serikali kwa matumizi ya ofisi ya umma.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bi. Mary Makondo, akipokea gari hilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, aliishukuru TRA kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha rasilimali zilizotaifishwa zinatumika kwa manufaa ya wananchi.

“Tunashukuru kwa msaada huu wa gari ambalo litasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kiutendaji katika Mkoa wa Ruvuma,” alisema Makondo.

Makabidhiano hayo ni sehemu ya jitihada za TRA za kuhakikisha sheria za kodi na forodha zinafuatwa kikamilifu, sambamba na kulinda maslahi ya taifa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • BARAZA la wazee la Makumbusho ya majimaji lachagua viongozi wake

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.