• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUENDELEE kupinga ukatili kwa Watoto- Waziri Mkuu Majaliwa

Imewekwa kuanzia tarehe: January 6th, 2024

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa jamii kuwa iendelee kuunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kupinga vitendo vya ukatili kwa watoto kwani vinasababisha watoto wengi kukimbia familia zao na kukosa makao maalum.

 “Jamii na Watanzania kwa ujumla kila mmoja ashiriki katika kulinda haki na ustawi wa watoto wetu. Hii ni nguvukazi ya Taifa letu hivyo basi, ulinzi na usalama wa watoto ni jukumu letu sote. Mamlaka zinazohusika ziendelee kusimamia, kufuatilia na kuratibu vyema huduma za Makao ya Watoto zinazotolewa na Serikali na wadau mbalimbali. “

 Ameyasema hayo leo Ijumaa, Januari 5, 2024, wakati wa hafla ya chakula cha mchana na watoto wanaolelewa katika makao ya kulelea watoto ya SWACCO yaliyoko Manispaa Songea mkoani Ruvuma, ambapo amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii watekeleze kikamilifu wajibu wao ikiwemo kutambua vituo au makao na kutatua changamoto za ustawi zinazoikabili jamii na kutoa msaada wa kisaikolojia na afya ya akili kwa walengwa.

 Pia, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wahakikishe wanaweka utaratibu wa kuwatembelea wadau wanaoshirikiana na Serikali kutoa huduma kwa wenye uhitaji ili kutambua changamoto walizo nazo na kuzitafutia ufumbuzi, pamoja na kuwapa uelewa wa mipango na mikakati ya Serikali kuhusu huduma za ustawi wa jamii.

 Kadhalika, Waziri Mkuu ameitaka wizara inayohusika na masuala ya ustawi wa jamii iendelee kushirikiana na wadau kuongeza kasi ya utoaji elimu ya malezi chanya kwa wazazi/walezi na jamii kwa ujumla ili kuwa na nguvu kazi yenye tija kwa Taifa. “Nawashukuru wadau na wafadhili kwa kusimamia Makao haya ili kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma stahiki za malezi na mahitaji muhimu. “

 Wakati huo huo, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania wote wahakikishe kuwa watoto wote wenye ulemavu wanapewa fursa ya kupata huduma za jamii ikiwemo elimu na waache tabia za kuwaficha ndani badala yake washirikishe mamlaka ikiwemo viongozi wa Mitaa, Vijiji, Kata na Wilaya ili kupata msaada.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.