• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU kushirikiana na TAWA kutatua changamoto za wanyama wakali

Imewekwa kuanzia tarehe: October 18th, 2024

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA Mabula Misungwi Nyanda akiongozana na Maofisa waandamizi wa Taasisi hiyo amekutana na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Kemori Chacha kwa ajili ya kujadili mustakabali wa utatuzi wa changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususani tembo inayowakabili wananchi wilayani humo.

Kamishna Mabula ameeleza namna Taasisi yake inavyotekeleza jukumu la kupambana na changamoto ya wanyamapori hao ili kuwaondolea adha wananchi na namna ilivyojipanga kutekeleza maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoyatoa akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Ruvuma Septemba, 2024 kuhusu kukabiliana na changamoto ya wanyamapori hao Katika wilaya za Tunduru na Namtumbo.

Mabula amesema TAWA inatarajia kuongeza vitendea Kazi ambapo Katika wilaya ya Tunduru itaongeza gari 1 na Pikipiki 2 zitakazotumiwa na Askari wahifadhi Kwa ajili ya mwitikio wa haraka wa matukio ya tembo, ikiwa ni pamoja na mabomu baridi 250 Kwa ajili ya kuwafukuza wanyamapori hao kutoka katika makazi ya watu.

Ili kuimarisha utendaji kazi, Kamishna Mabula amesema TAWA imejenga kituo cha Askari wa kudumu eneo la Chingulungulu na hivi karibuni itaongeza idadi ya Askari wahifadhi wapatao 20 Katika kituo kidogo cha Songea ili kuwaongezea nguvu Askari 8 waliopo sasa wilayani Tunduru ikienda sambamba na kuanzisha kituo cha muda cha Askari katika tarafa ya Namasakata.

Katika hatua nyingine Kamishna Mabula ametumia ziara hiyo kuongea na Maafisa na Askari wa uhifadhi ili kusikiliza changamoto wanazopitia Katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhimiza utendaji Kazi unaozingatia Sheria, kanuni na taratibu ikiwa ni pamoja na kusisitiza ushirikiano na vyombo vingine vya dola hususani Jeshi la Polisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Kemori Chacha amepongeza jitihada zinazofanywa na TAWA na Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa ujumla wilayani humo Katika kukabiliana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususani tembo na kusisitiza kuendelea kutoa elimu ya kujikinga na madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori hao Kwa wananchi

 Pia ametilia mkazo suala la ushirikiano baina ya Halmashauri, Taasisi za uhifadhi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na wadau wa uhifadhi Katika kutekeleza Mkakati wa Wizara wa kukabiliana na migongano baina ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.