• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Tunduru wanavyonufaika na stakabadhi ghalani,waingiza bilioni 17

Imewekwa kuanzia tarehe: July 15th, 2023

WAKULIMA wa zao la ufuta wilayani Tunduru,wamefanikiwa  kuingiza Sh.bilioni 17,131,112,080.6 baada ya kuuza tani 4,641 sawa na kilo milioni 4,641,473.7 za ufuta ghafi kupitia minada 6 iliyofanyika kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani wilayani humo.

Hayo yamesemwa j na Afisa Masoko wa Chama Kikuu cha Ushirika(TAMCU Ltd) wilaya ya Tunduru Marcelino Mrope kwenye mnada wa sita wa zao hilo uliofanyika katika Chama cha msingi cha Ushirika Mlimi(Amcos)kijiji cha Misechela.

Alisema,katika mnada wa sita uliofanyika kijiji cha Misechela wakulima wameuza zaidi ya tani 240.8  za ufuta sawa na kilo 240,818.5 zenye thamani ya Sh.milioni 836,362,650.5.

Aidha alisema,katika mnada wa tano uliofanyika kijiji cha Namwinyu jumla ya tani 770  za ufuta wenye thamani ya Sh.bilioni 2,678,000.00 uliingizwa sokoni ambapo bei ya wastani ilikuwa Sh.3,475 kwa kilo moja.

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika TAMCU Ltd Mussa Manjaule,amewapongeza wakulima kwa kubuni mazao mbadala ya biashara ikiwemo zao la ufuta ambalo limewaingizia fedha nyingi katika kipindi kifupi.

Alisema,hatua hiyo  ni mafanikio makubwa  na kuwasisitiza kulima kilimo cha kisasa kwa kufuata maelekezo ya wataalam na kuongeza ukubwa wa mashamba yao ili kujikomboa na umaskini kupitia shughuli zao za kilimo.

Manjaule amewataka wakulima wa ufuta na mazao mengine,kutumia fedha wanazopata kufanya mambo ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba za kisasa na kusomesha watoto wao na kuepuka kutumia fedha kwenye mambo ya anasa ambayo ni adui mkubwa wa maendeleo.

Naye Afisa Ushirika wa wilaya ya Tunduru Geroge Bisan  alisema,zao la ufuta limeendelea kufanya vizuri kutokana na uzalishaji wake kuongezeka mwaka hadi mwaka hali iliyopelekea hata bei kuwa nzuri ikilinganisha na miaka ya nyuma.

Amewasihi wakulima kutumia ardhi yao vizuri kwa kuongeza uzalishaji wa mazao mashambani na kuepuka kuuza ardhi ovyo  kwa wageni  walioanza kuingia kwa wingi katika wilaya hiyo kutafuta ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo na biashara.

Badala yake waitumie wao wenyewe kuzalisha kwa wingi mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama njia pekee ya kuondokana na umaskini kwenye familia zao.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima wenzake Kitanda Rashid,ameipongeza serikali kusimamia uuzaji wa zao la ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani kwani umekuwa mkombozi mkubwa kwa wakulima.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.