• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU wazindua kampeni ya kutokomeza kifua kikuu

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2022

SERIKALI kupitia Hospitali ya wilaya ya Tunduru kitengo cha Kifua Kikuu na Ukoma, imezindua rasmi kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu mwaka 2022 kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kutokana na kundi hilo kuwa katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya ugonjwa huo.

Katika kampeni hiyo yenye kauli mbiu “kila unayemuona mbele yako ni mhisiwa wa kifua kikuu” itaenda sambamba kwa kuwapima na kuwaanzia dawa watoto wote watakaobainika kuwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa TB.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa wilaya,Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wilaya ya Tunduru Dkt Mkasange Kihongole alisema,kampeni hiyo ni endelevu na lazima kwa watoto wote walio chini ya umri huo.

Dkt Kihongole alisema,wataalam wa kitengo cha kifua kikuu na ukoma Hospitali ya wilaya Tunduru watazunguka kila kijiji kwa ajili ya kutoa elimu ya kifua kikuu,kufanya uchunguzi na kuwaanzishia matibabu watakaobainika kuwa na dalili za kifua kikuu.
Alisema, katika mkoa wa Ruvuma wilaya ya Tunduru inatajwa kuongoza kuwa na wagonjwa wengi wa kifua kikuu ambapo kwa mwaka 2021, jumla ya watu 769 waliobainika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo.

Alisema,kifua kikuu ni ugonjwa unaoambikizwa kwa njia ya hewa ambapo mtu mwenye ugonjwa huo anapokohoa bila kuziba mdomo ni rahisi sana kuwaambukiza wengine.Kihongole alitaja dalili za ugonjwa huo kwa watoto wadogo ni kupungua na kutoongezeka uzito,homa za mara kwa mara,kulia lia na makuzi duni

Amewataka wazazi na walezi, wanapoona dalili hizo kwa watoto ni vyema kuwapela Hospitali na vituo vya afya vilivyopo katika maeneo yao kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalam.
Aidha alitaja dalili kwa watu wazima ni kukohoa kwa muda wa wiki mbili na zaidi,kukohoa damu,kutoka jasho usiku wa manane,kukonda na kupoteza hamu ya kula.

Kihongole,ameyataja makundi yaliyo katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa huo ni watoto wadogo,wazee,watu wanaoishi na virusi vya ukimwi,wanaokunywa pombe kupita kiasi,wasafiri na wanaoishi na kukaa kwenye mikusanyiko kama wanafunzi wanaoishi bweni na wafungwa.

Amina Jinga,amepongeza jitihada za serikali katika kupambana na ugonjwa huo kwani zitawasaidia wazazi na walezi kufahamu afya za watoto wao na kuchukua hatua pale watakapobainika kupata na ugonjwa huo.

Secilia Komba,ameiomba Serikali kupitia wataalam wake kutembelea mara kwa mara maeneo ya vijijini kwa ajili ya kutoa elimu ya magonjwa mbalimbali ikiwamo TB kwa sababu maeneo mengi hayo wananchi hawana elimu ya kutosha kuhusu kifua kikuu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.