• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU yazindua mkakati wa kutokomeza kifua kikuu

Imewekwa kuanzia tarehe: February 20th, 2022

HOSPITALI ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na shirika la usimamizi na uboreshaji wa huduma za afya(MDH) imezindua mkakati wa kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu kwa kutoa vifaa vya kukusanyia sampuli za makohozi kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

Mratibu wa MDH Dkt Nikson John alisema, vifaa hivyo vilivyotolewa kwa wahudumu wa afya ni kuunga mkono juhudi za Serikali na zinalenga kusaidia katika kampeni ya kutokomeza ugonjwa huo ambao bado umekuwa tatizo kwa jamii hasa wanaoishi maeneo ya pembezoni.

Dkt Nikson alisema,MDH mkoa wa Ruvuma inasaidia eneo la kifua kikuu kwa kutoa vifaa na kuwawezesha wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu ambapo amevitaja vifaa hivyo ni wahudumu hao ni makoti ya mvua,buti, na vifaa vya kukusanyia sampuli za makohozi.
Alisema, vifaa hivyo vinakwenda kuongeza hamasa kwa wahudumu hao pamoja na kuleta tija katika kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu inayofanywa na Hospitali ya wilaya kupitia kitengo cha kifua kikuu na ukoma.


Kwa upande wake,Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa wilaya ya Tunduru Dkt Mkasange Kihongole amewashukuru wadau Shirika la MDH kwa kutoa vifaa ambavyo vitasaidia katika kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu hasa wakati huu wa masika ambapo Jiografia ya wilaya hiyo sio rafiki kwa wahudumu hao ambao wanakwenda katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao.

Alisema, vifaa hivyo vitawapa morali wahudumu hao kwa kufanya kazi katika mazingira yoyote bila kujali mvua au jua ambapo lengo la wilaya hiyo ni kufanya vizuri katika mapambano ya ugonjwa wa huo chini ya kauli mbiu kila unayemuona mbele yako ni “muhisiwa wa kifua kikuu”.

Alisema, vifaa hivyo vilivyotolewa katika kitengo cha kifua kikuu na ukoma vitaleta ufanisi mkubwa kwa kuibua wahisiwa wengi, kwani unapopata idadi kubwa ya wahisiwa ni dhahiri hata wagonjwa wataongezeka.

Dkt Kihongole alisema,lengo la wilaya hiyo ni kuendelea kuibua wagonjwa wengi ambao wataanzishiwa matibabu ili wilaya ya Tunduru ibaki salama bila maambukizi ya ugonjwa huo.

Naye muhudumu wa afya ngazi jamii Iddi Yakiti(Nyuki) amelishukuru Shirika la MDH kwa kutoa vifaa hivyo ambavyo vinakwnda kusaidia katika kazi ya kukusanya sampuli za makohozi vijijini na kuleta vituoni kwa ajili ya uchunguzi.

Alisema, awali utendaji wa majukumu yao ulikuwa mgumu kwani wakati mwingine walinyeshewa na mvua na kusababisha hata sampuli za makohozi nazo kulowa jambo lililosababisha kushindwa kufikia malengo yao.
MWISHO.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.