• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUZO mbili za Rais zilizokabidhiwa kwa RC Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 14th, 2022

MKUU  wa Mkoa  wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekabidhiwa Tuzo mbili zilizotolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kampuni ya DAN AND ASSOCIATES ENTERPRISES LTD (DAE LTD)kutoka Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma .

Akizungumza kabla ya kukabidhi Tuzo hizo kwa Mkuu wa Mkoa katika hafla iliyofanyika kwenye Ofisi za Kampuni hiyo mjini Mbinga,Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya DAN AND ASSOCIATES ENTERPRISES LTD (DAE LTD) Dastan Komba amesema,Kampuni hiyo imekuwa kinara kitaifa wa kupata Tuzo zinazotolewa na Rais katika sekta ya viwanda kwa miaka miwili mfululizo mwaka 2021 na 2022. 

“Kampuni ya DAE Ltd imeweza kuwa mshindi bora wa kiwanda cha kati cha uchakataji wa chakula Tanzania (Winner of 2021/2022 Food Processing Medium Scale) kwa miaka miwili mfululizo “,alisema Komba.

Amevitaja vigezo saba vinavyozingatiwa ili kupewa tuzo hizo kuwa ni kiwanda kuzingatia mnyororo mzima wa uchakataji na kiwanda kuzingatia taratibu za ajira na ulipaji mishahara.

Vigezo vingine amevitaja kuwa ni kiwanda kulipa kodi zake zote,matumizi bora ya nishati ya umeme,matumizi ya teknolojia,utunzaji mazingira na matumizi ya vifaa vya kujikinga na Usalama. 

Amesema kampuni ya DAE yenye wafanyakazi 150 inamiliki kiwanda cha kahawa,ina miliki hekari 40 zenye miche ya kahawa 20,000 na mitambo 42 ya kuchakata kahawa. Mkurugenzi huyo wa DAE amesema baada ya Rais kumkabidhi Tuzo hizo na yeye ameamua kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa sababu zimeleta heshima kubwa kwenye Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas baada ya kukabidhiwa tuzo hizo amempongeza Mkurugenzi wa DAE kwa kupewa Tuzo mara mbili mfululizo na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Hata hivyo amesema tuzo hizo zimetolewa kwa lengo la kutambua mchango wa Kampuni ya kizalendo katika uzalishaji wa bidhaa za viwandani zenye viwango vya kati.

“Sisi kama Mkoa mafanikio haya tunaona ni fahari kubwa kwetu “,alisisitiza Kanali Thomas.

Licha ya kukabidhiwa tuzo hizo Mkuu wa Mkoa pia alitembelea kiwanda cha Kahawa cha Mwekezaji huyo ambapo ametoa rai kwa wawekezaji wengine kuiga mfano wa kampuni ya DAE LTD iliyofanya uwekaji mkubwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Ndugu Oddo Mwisho amesema tuzo hizo zilizotolewa kwa Mwekezaji Mzawa zinadhihirisha kuwa serikali inawajali wawekezaji wa ndani.

Kampuni ya DAE LTD yenye wafanyakazi 150 ilianzishwa mwaka 1988.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya MKuu wa Mkoa wa Ruvuma

Desemba 14,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.