• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UFAHAMU utalii wa mambokale na ujio wa dini wilayani Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 11th, 2024

 vivutio vya mambokale  vinapaswa kupewa kipaumbele kwa sababu vinachangia katika kukuza historia na kuendeleza utalii.Wilaya ya Nyasa imebarikiwa pia na utalii wa mambokale ambao unavutia wengi kujua masuala mbalimbali ya kihistoria katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Vivutio vya mambokale katika wilaya ya Nyasa vimegawanyika katika sehemu ambazo ni historia za mambokale zilizofanywa na viongozi wa nchi  katika maeneo mbalimbali na kuingia kwa dini na madhehebu ambayo yameacha alama kubwa. 

Baadhi ya vivutio vya mambokale katika wilaya ya Nyasa  ni kile kilichopo  Katika  eneo la  Mbamba bay ambapo  Rais Mstaafu wa Awamu ya Kwanza Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Oscar Kambona katika harakati za kudai Uhuru walilala hapo miaka ya 1956 nyumbani kwa dada wa Oscar Kambona ambapo palikuwa na ofisi ya chama cha TANU.

 Magavana wa Shirikisho wa Rodesia na Nyasaland walikutana katika (Rest House) eneo la Mbamba bay jengo ambalo kwa sasa ni ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Mbambabay wakiwa na lengo la kuagana kutokana na vuguvugu la waafrika kudai Uhuru 1959 kushika kasi. Jengo hilo lilijengwa kwa miti.

Kivutio kingine cha utalii wa mambokale ni Kuingia kwa dini  na madhehebu mbalimbali pia  sehemu kubwa ya utalii wa nyasa unaobeba historia.

Mwaka 1981 wananchi wa Lituhi waliahamishwa kwa ajili ya kupisha mafuriko yaliyosababishwa na kufungwa kwa Mto Shire nchini Malawi na baadaye mwaka 1987 Mwalimu Nyerere akiwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi alifika kwa ajili ya kutoa maamuzi magumu ya kuwarudisha katika makazi yao ya awali na baada ya kuongea na wananchi hao kwenye mti mtebhele (muyombo) ambao upo katika kijiji cha Mwera mpya kata ya Lituhi na baadae alipiga picha na mkewe katika eneo hilo kabla ya kuondoka. 

Dini iliyoanza kuingia katika wilaya ya Nyasa ni dini ya Kikristo,Mwinjilisti wa kwanza wa Anglikana William Parcival Johnson alianza kuhubiri Februari 9,1881 na akahamia rasmi Liuli mwaka 1906, alifariki Oktoba 11,1928 na kuzikwa Liuli.

Wakati huo ilitambulika kwa jina la DayosisI ya Nyasaland, ikafuata Dayosisi ya Southwest Tanganyika mwaka 1952 na baadaye kuitwa Dayosisi ya Ruvuma  mwaka 1971.

Mwinjilisti William Parcival Johnson awali wakati anaingia Nyasa alikuwa na lengo la kujenga kanisa Kijiji cha Hongi ambapo wenyeji hawakutaka na alifukuzwa ndipo akakilaani kijiji cha Hongi kiwe na sisimizi wengi, pia kiote majani yaitwayo mapelele ambayo kabla yake hayakuwapo. Historia na simulizi za wahenga zinatoa simulizi hizo za kusisimua.

Historia inaonesha kuwa Kanisa Katoliki wilayani Nyasa liliingia mwaka 1912 huko Nkaya na kuanzisha Parokia na baadae kujenga kanisa kubwa la Lituhi mwaka 1939. Mwanzilishi akiwa ni Padre Henrich Kunster.

 Uislamu uliingia Nyasa mnamo mwaka 1928, Sheikh wa kwanza aliitwa Mzee Bin Amanzi, Ilipofika mwaka 1932 Waasisi walijenga msikiti ambao miongoni mwao ni Twaib Abdallah, Akida Wabu, Mdoka, Ajali Hassan, Mfaume Bolin na Issa Kimambe.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.