• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UFUTA wawaingizia wakulima Ruvuma bilioni 25

Imewekwa kuanzia tarehe: February 11th, 2021

WAKULIMA mkoani Ruvuma wamefanikiwa kuingiza zaidi ya shilingi bilioni 25 baada ya kuuza kilo 12,234,757 ya zao hilo kupitia mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani kuanzia msimu wa mwaka 2018/2019 hadi 2019/2020.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema katika kipindi hicho wakulima pia walifanikiwa kuuza kilo 1,499,077  za zao la soya zilizowaingizia zaidi ya shilingi bilioni moja na zao la mbaazi ambalo liliwaingizia zaidi ya shilingi bilioni 2.585 baada ya kuuza kilo 4,260,777.

“Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa ambayo imekuwa inatekeleza mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani,pia tuna mazao mawili ya kimkakati ambayo ni korosho na kahawa,yamekuwa yakiuzwa kupitia mfumo huu’’,alisema Mndeme.

Amesema mfumo huo umewanufaisha wakulima kwa kupata soko la uhakika na bei nzuri ya mazao yao na kwamba shughuli za kilimo katika msimu wa mwaka 2020/2021 zinaendelea vizuri ambapo wakulima wamelima mazao mbalimbali.

Kuhusu mbolea,Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mbolea Tanzania(TFRA) unaendelea kusimamia upatikanaji wa mbolea ili wananchi waweze kuzalisha chakula cha kutosha.

Hata hivyo amesema hadi kufikia Novemba 2020 jumla ya tani 31,624 za mbolea zilikuwa zimeingia mkoani Ruvuma kati ya mahitaji ya mbolea tani 50,524.50.

Mkoa wa Ruvuma umekuwa gwiji katika uzalishaji wa mazao ya chakula nchini,baada ya kushika nafasi ya kwanza kitaifa miaka miwili mfululizo,msimu wa mwaka 2018/2019 na 2019/2020.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 11,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.