• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI wa chuo cha Uhasibu Arusha,Kampasi ya Songea,ndoto ya Rais Samia yatimia

Imewekwa kuanzia tarehe: April 1st, 2025

Katika juhudi za kuboresha elimu ya juu nchini Tanzania, ndoto ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila mkoa unakuwa na chuo kikuu inaendelea kutekelezwa kwa vitendo.

Mkoa wa Ruvuma sasa utajivunia kuwa mwenyeji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa tawi la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika Manispaa ya Songea.

Kwa mujibu wa Meneja wa Chuo cha Uhasibu Arusha Kampasi ya Songea, Dkt. Bakari Mashaka, ujenzi wa chuo hicho unatarajiwa kugharimu takribani shilingi bilioni 18.5, fedha ambazo zimetolewa na serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Chuo hiki kipya kitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 10,000 wa programu mbalimbali, jambo linaloashiria mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu na uchumi wa mkoa wa Ruvuma.

Safari ya Chuo cha Uhasibu Songea

Kwa sasa, IAA Kampasi ya Songea inatoa huduma zake katika jengo la TTCL, ghorofa ya pili, mjini Songea. Kozi zinazotolewa ni pamoja na Diploma ya Usimamizi wa Biashara, Uhasibu, TEHAMA, Fedha na Benki, pamoja na masomo ya ngazi ya uzamili katika fani za Biashara, Fedha, TEHAMA, Uongozi na Usimamizi wa Rasilimali.

Katika mahojiano maalum, Dkt. Mashaka alifafanua kuwa chuo hicho kinajikita katika kuwaandaa wanafunzi kwa ujuzi wa vitendo, hasa katika ujasiriamali ambapo amelitaja lengo kuu ni kuhakikisha wahitimu hawategemei tu ajira, bali wanakuwa wabunifu na wajasiriamali wa kujitegemea.

Fursa kwa Wananchi

Afisa Uhusiano wa IAA Kampasi ya Songea, Nuru Meshack, ameeleza kuwa baadhi ya wazazi huamini kuwa mwanafunzi aliyepata daraja la nne katika mtihani wa kidato cha nne hawezi kuendelea na masomo.

Hata hivyo anafafanua kuwa ufaulu wa daraja la nne (isipokuwa katika masomo ya dini) unaruhusu mwanafunzi kujiunga na chuo, hivyo akawahamasisha vijana kuchangamkia fursa zilizopo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Dkt. Mwaitete Cairo, ameishukuru Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kutoa eneo la hekari 71 kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu hicho.

Amesisitiza  kuwa ujenzi  wa chuo kikuu hicho utaanza mara moja kwa kutumia mfumo wa ‘force account’, hivyo wananchi wa Songea wanapaswa kujiandaa kupata nafasi za ajira na fursa za kibiashara zitakazotokana na mradi huu.

Mchango wa Ujenzi kwa Maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma

Eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo hiki lipo katika kata ya Tanga, likizungukwa na maeneo muhimu ya kiuchumi kama vile Stendi Kuu ya Mabasi ya Tanga, Machinjio ya Kisasa na Hospitali ya Rufaa ya Manispaa ya Songea.

Hii inaashiria kuwa uwekezaji huu hautasaidia tu elimu, bali pia utachochea maendeleo ya kiuchumi kwa wakazi wa Songea na mkoa mzima wa Ruvuma.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Michael Mbano, amepongeza uongozi wa Chuo cha Uhasibu Arusha kwa hatua hii muhimu, akisema kuwa wamejibu kilio cha wananchi  wa  Mkoa wa Ruvuma kutaka taasisi za elimu ya juu mkoani humo.

Kwa jumla, ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha Kampasi ya Songea si tu utasaidia kuinua kiwango cha elimu, bali pia utafungua milango ya maendeleo na ajira kwa wakazi wa Songea na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Wakati huo huo cha Uhasibu Arusha (IAA), kimejipanga kufanya maboresho Makubwa ili kwendana na mabadiliko ya teknolojia kwa kuanza kutumia madarasa mtandao ili kuwezesha kutoa elimu kwa kundi kubwa la wanafunzi maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi

Madarasa hayo ya kisasa yatamwezesha mwalimu atakayekuwa kwenye chumba cha darasa katika kampasi zake Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Babati mkoani Manyara na Songea na nchi watakazofungua matawi Sudan Kusini na Comorro kusoma kwa wakati mmoja.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.