• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI wa kituo cha afya Mtakanini Namtumbo wafikia asilimia 95

Imewekwa kuanzia tarehe: June 12th, 2020

UBORESHAJI wa kituo cha afya Mtakanini katika Halmasauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ,ambao serikali ilitoa sh.milioni 400  umefikia asilimia 95.

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Dr.Godwin Luta akitoa taarifa ya  kituo hicho kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,amesema ujenzi wa kituo hicho ni utekelezaji wa Ilani ya CCM wa kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya.

Amesema kiasi hicho cha fedha kimetumika kujenga jengo la wagonjwa wa nje,maabara,choo cha wagonjwa wa nje,jengo la kufulia,chumba cha upasuaji na ukarabati wa jengo la mama na mtoto.

“Mradi huu utakapokamilika kwa asilimia 100,tutakuwa tumewapunguzia wananchi kero ya kusafiri umbali mrefu wa kutafuta huduma ya afya na upasuaji nje ya Halmashauri ya Namtumbo’’,alisisitiza.

Hata hivyo amesema hadi sasa zimetumika zaidi ya Sh.milioni 300 kutekeleza mradi huo na kwamba zimebaki shilingi milioni 95 kwa ajili ya kukamilisha majengo hayo.

Akizungumza mara baada ya kukagua majengo ya kituo hicho,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewapongeza  wananchi hao kwa kufikia hatua kubwa ya ujenzi unaotarajia kukamilika hivi karibuni.

Amesema serikali kwa wakati mmoja ilitoa fedha kiasi cha shilingi  bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa  vituo vya afya vitatu mkoani Ruvuma, ambavyo ni Mgagagura,Mtakanini na Matimira.

Hata hivyo amesema vituo vingine bado havijaanza  ujenzi wakati kituo cha afya Mtakanini kipo katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi.

Amesema ataviagiza vituo vingine ambavyo bado havijatekeleza mradi huo kufika kujifunza katika kituo cha afya Mtakanini kutokana na kufanya kazi nzuri ya ujenzi wa majengo sita na fedha imebaki.

“Kwa kuwa ujenzi unakwenda mwisho,nakuomba Mkurugenzi uanze mchakato wa manunuzi wa vifaa vya kituo hiki,vikiwemo vitanda, madogoro, mashuka,dawa na vifaa vingine vinavyotumika katika huduma ya afya’’,alisisitiza.

Mndeme pia amewaagiza RUWASA wilaya ya Namtumbo kupeleka maji katika kituo hicho, TANESCO kupeleka huduma ya umeme na TARURA  kukamilisha matengenezo ya barabara haraka.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 12,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.