• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UKIMWI bado tishio Ruvuma ,watu zaidi ya 68,000 wanaishi na VVU

Imewekwa kuanzia tarehe: April 1st, 2025

Katika mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), Mkoa wa Ruvuma umeonesha hatua kubwa za maendeleo katika kupunguza maambukizi na kuboresha huduma kwa waathirika.

 Takwimu za hivi karibuni zinaonesha kuwa mwaka 2024, Ruvuma inakadiriwa kuwa na watu wanaoishi na VVU (WAVIU) 68,237. Kati yao, wanaume ni 24,959 (asilimia 37) huku wanawake wakiwa 43,238 (asilimia 63).

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Luois Chomboko anasema Watoto walio na umri chini ya miaka 15 ni 2,382 (asilimia 3.5), huku watu wazima wenye umri wa miaka 15 na kuendelea wakifikia 65,855 (asilimia 96.5).

Kwa upande wa halmashauri, Manispaa ya Songea inaongoza kwa idadi kubwa ya WAVIU ikiwa na watu 18,398, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru yenye watu 9,888, na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ikiwa na watu 9,003.

Kupungua kwa Maambukizi Mapya ya VVU

Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Mkoa wa Ruvuma ni kupungua kwa kiwango cha maambukizi mapya ya VVU.

 Idadi ya maambukizi mapya imeshuka kwa watu 279, sawa na asilimia 28.6, kutoka watu 2,168 mwaka 2023 hadi 1,889 mwaka 2024.

Wanawake wanaendelea kuathirika zaidi, wakihusisha asilimia 64.8 ya maambukizi yote (watu 1,225), huku vijana wa umri wa miaka 15-24 wakiwa na maambukizi 651 (asilimia 34).

 Kwa watoto walio chini ya mwaka mmoja, maambukizi mapya yamefikia 168, sawa na asilimia 9.

Hatua Kubwa Katika Udhibiti wa VVU

Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kutekeleza afua mbalimbali za kudhibiti maambukizi ya VVU, ikiwa ni pamoja na Kupungua kwa kiwango cha maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 12.9, kutoka watu 3,168 mwaka 2022 hadi 1,889 mwaka 2024,WAVIU 57,421 (asilimia 84.1) wanajua hali zao za maambukizi,WAVIU 57,160 (asilimia 99.5) wanatumia dawa za kufubaza makali ya VVU na WAVIU 55,445 (asilimia 97.2) wamefanikiwa kufubaza VVU kwa kiwango kinachopunguza hatari ya maambukizi mapya.

Kupungua kwa Vifo na Unyanyapaa

Mafanikio mengine makubwa ni kupungua kwa idadi ya WAVIU waliopotea katika matibabu, kutoka watu 1,472 (asilimia 2.5) mwezi Aprili 2024 hadi 300 (asilimia 0.5) mwezi Desemba 2024.

 Aidha, idadi ya vifo miongoni mwa WAVIU imepungua kutoka vifo 11 kwa kila watu 1,000 mwaka 2020 hadi kifo 1 kwa kila watu 1,000 mwaka 2024.

Kiwango cha unyanyapaa dhidi ya WAVIU pia kimepungua kutoka asilimia 64.5 mwaka 2012 hadi asilimia 25.5 mwaka 2024, hatua ambayo inatoa matumaini makubwa kwa jamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

    May 31, 2025
  • WAKULIMA Namtumbo wachuma neema ya ufuta kwa teknlojia mpya ya mnada wa kidigitali

    May 31, 2025
  • RUSHWA yazidi kuporomoka na kukosa nafasi Ruvuma

    May 31, 2025
  • SERIKALI yatoa fidia ya bilioni 2.5 kupisha mradi wa umeme wa Grid Songea-Tunduru

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.