• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UMEME wa REA kuwashwa Nalasi Tunduru Agosti 30 mwaka huu

Imewekwa kuanzia tarehe: August 8th, 2021

WAZIRI wa nishati Dkt Medard Kalemani, amezindua ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme vijijini(Rea) wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, na kutoa  mwezi mmoja  hadi tarehe 30 Agosti  wakandarasi wa miradi hiyo kukamilisha kazi  kwa muda uliopangwa.

Amewataka wakandarasi wanaojenga mradi huo, kuhakikisha wanapeleka umeme katika vijiji vyote  vilivyopangwa kufikiwa na mradi huo wa awamu ya tatu kwa kuwa wananchi wana hamu kubwa  ili waweze kuutumia katika shughuli za uzalishaji.

Dkt Kalemani, ametoa agizo hilo jana wakati wa uzinduzi wa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa pili  katika kijiji cha Nalasi wilaya ya Tunduru.

Dkt Kalemani amesema, suala la kuunganisha umeme hapa nchini sio hiari  bali ni jambo la lazima,ndiyo maana Serikali imedhamiria kufikisha umeme katika vijiji vyote ambavyo vilisahaulika kwenye  awamu mbili zilizopita katika wilaya hiyo.

Amewahidi wananchi na viongozi wa wilaya ya Tunduru kuwa,vijiji vyote vilivyobaki vinakwenda  kupata umeme ndani ya mwezi mmoja kwa kuwa  Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeshatoa fedha  za kutekeleza mradi huo.

Amesema,mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa pili katika wilaya ya Tunduru umepangwa kufikishwa katika vijiji 85 na kuwasisitiza wakandarasi kutoruka hata kijiji kimoja  wakati wa utekelezaji wa utekelezaji wake.

Dkt Kalemani amewaagiza viongozi wa shirika la umeme Tanesco wilaya ya Tunduru,kufungua ofisi ndogo katika kijiji cha  Nalas ili  wananchi  wasiangaike kwenda hadi Tunduru  mjini kwa ajili ya kulipia gharama za kuunganishiwa umeme kwenye makazi yao.

Aidha, amewakumbusha viongozi wa Serikali za vijiji kutenga maeneo maalum ya uwezekaji ili yaweze kupelekewa miundombinu ya umeme wakati wa utekelezaji wa mradi  wa kusambaza umeme vijijini.

“nawaomba sana viongozi wa serikali za vijiji kutenga maeneo  ya  uwekezaji ili yapelekewa umeme na tumieni umeme utakaoletwa kufanya biashara na kuongeza thamani ya mazao yenu ya kilimo na mifugo na kuanzisha viwanda vidogo na vikubwa”amesema Dkt Kalemani.

Amesema, miradi ya kusambaza umeme katika vijiji vilivyosahaulika ndani ya mkoa wa Ruvuma utatekelezwa kwa muda wa miezi 18 na Serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 71na unatekelezwa na wakandarasi watatu ili kuharakisha utekelezaji wake.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge ameishukuru Serikali kupitia wizara ya nishati kuanza ujenzi wa mradi huo ambao unakwenda kuharakisha uchumi wa mkoa wa Ruvuma.

Aidha, amekemea tabia ya baadhi ya watu wanaohujumu na kuiba miundombinu ya umeme  na kuwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu kwa kuwafichua watu  wanaojihusisha na vitendo hivyo.

“tunaleta umeme wana Nalasi, maeneo mengine ambako umeme unapita wameanza kujisahau wanaiba nyaya,yaani juhudi  na fedha zote zaidi ya bilioni 71.1 zimeletwa kwa ajili ya Ruvuma pekee yake  ikiwemo hapa  Nalasi, lakini  kichaa mwingine  kwa maslahi yake anajiamulia    kwa kuiba nyaya za umeme,tabia hiyo inarudisha nyuma juhudi za Serikali za kuwaletea  maendeleo”amesema Jenerali Ibuge.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini Daimu Mpakate amesema, jimbo la Tunduru kusini lina vijiji 65 lakini  vilivyofikiwa na umeme ni 12 tu ambapo ameiomba wizara ya nishati kukamilisha kazi hiyo haraka ili wananchi watumie umeme huo kujiletea maendeleo.

Imeandikwa na Muhidin Amri,Tunduru


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.