• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

USAMBAJI wa ripoti ya UKIMWI wazinduliwa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: November 30th, 2024

Waziri wa Afya, Mheshimiwa Jenista Mhagama, amezindua usambazaji wa ripoti ya utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI kwa mwaka 2022/23 mkoani Ruvuma.

Uzinduzi huo umefanyika katika Kongamano la Kitaifa la Kisayansi lililofanyika katika ukumbi wa Chandamali mjini Songea, ikiwa ni sehemu ya matukio muhimu kuelekea maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani, Disemba Mosi,  ambayo yatafanyika mkoani hapo.

Katika uzinduzi huo Mhe. Jenista amesisitiza kuongeza bidii katika kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

"Kiwango cha ushamari wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kimepungua kitaifa kutoka 7% mwaka 2003/2004 mpaka 4.4% mwaka 2022/23, jambo lingine ambalo tunatakiwa kujipongeza lakini tunatakiwa kuongeza bidii ni kiwango cha maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ambacho nacho kimepungungua kutoa 18% mwaka 2010 hadi 8.1%  mwaka 2023.

Amehimiza kila mmoja kulinda mafanikio yaliyopatikana na kuhakikisha Taifa linafanya vizuri zaidi katika mapambano dhidi ya UKIMWI, na amewataka TACAIDS kuendelea kuweka utaratibu wa kusikiliza na kutatua malalamiko yanayotokana na unyanyapaa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), John Kamwela amesema utafiti huo uliofanyika ni hatua muhimu katika kutoa taswira halisi ya nchi katika kufikia malengo ya kimataifa ya kumaliza janga la UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

Amesema majibu ya utafiti huo yatasambazwa katika ngazi za mikoa na wilaya ili kuwezesha watu wa maeneo hayo kupata taarifa za utafiti na kuboresha utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI katika maeneo hayo.

Mtakwimu Mkuu wa Zanzibar, Salum Kasssim Ali, akizungumza kwa niaba ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Tanzania Dkt. Albina Chuwa amesema takwimu rasmi zilizotokana na utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI kwa mwaka 2022/23 zitatumika kupanga dhima na kutekeleza mipango ya kitaifa na kimataifa na kufuatilia programu mbalimbali katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Utafiti huo umesimamiwa na Serikali ya Tanzania kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) na Zanzibar (ZAC), ukiratibiwa na Ofisi za Takwimu Tanzania (NBS) na Zanzibar (OCGHS), na kufadhiliwa na PEPFAR na kupata msaada wa kiufundi kutoka CDC na Shirika la ICAP la Chuo Kikuu cha Columbia, Marekani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.