• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

USHIRIKA ulivyopandisha mauzo ya kahawa Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: July 18th, 2022

Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma (MBIFACU) kimefanikisha ukusanyaji wa zao la kahawa kavu hadi kufikia zaidi ya tani 20,000 katika msimu wa mwaka 2021/2022.

Akizungumza wakati anatoa taarifa ya MBIFACU kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini Asangye Bangu,Kaimu Meneja wa MBIFACU Henerick Ndimbo amesema katika msimu wa mwaka 2021/2022 bei ya kahawa katika vyama vyote vya msingi imepanda hadi kufikia zaidi ya shilingi 7,000/= kwa kilo.

Amesisitiza kuwa Mfumo wa stakabadhi ghalani umeleta faida nyingi kwa mkulima ikiwemo kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo na kwamba katika kipindi cha miaka mitatu ushirika katika Wilaya ya Mbinga unaendelea kuimarika.

Faida nyingine ambazo wakulima wamezipata kupitia mfumo huo amezitaja kuwa ni kupunguza mfumo wa kilanguzi,kuanzishwa minada ya kikanda ya kahawa na wanachama kwenye vyama vya Msingi kupata Bima ya afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini Asangye Bangu amekipongeza Chama kikuu cha Ushirika Mbinga  kwa kuimarisha Ushirika.

"Lengo la ziara yetu ni kukutana na wakulima ili kujionea wenyewe changamoto na mafanikio katika utekelezaji wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nichukue fursa hii kuwapongeza Mbinga mnafanya kazi nzuri inayoheshimika ",alisema Bangu.

Ameahidi kutafutia ufumbuzi changamoto zinazotokana na utekelezaji Mfumo wa stakabadhi ghalani ikiwemo ya kuchelewa kwa malipo na upungufu wa pembejeo za kilimo ambazo hazikidhi mahitaji ya wakulima.

Akizungumza na wakulima wa kahawa katika Chama cha Msingi Mahenge Mbinga Mkurugenzi huyo wa stakabadhi ghalani amewapongeza wananchi hao kwa kuanzisha miradi mbalimbali iliyotokana na mfumo wa stakabadhi ghalani ikiwemo kuanzisha Shule ya sekondari na miradi ya utengenezaji sabuni na batiki.

Naye Afisa Kilimo Mkoa wa Ruvuma Onesmo Ngao Akizungumza na wakulima wa Chama cha Msingi Mahenge ameagiza kila chama cha Msingi cha Ushirika kuanzisha kitalu chake cha miche ya kisasa ya kahawa.

Amesema uzalishaji wa miche ya kahawa utawezesha kufikia lengo la la kitaifa la kuzalisha tani laki tatu za kahawa.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa nchini ambayo inatekeleza kwa mafanikio makubwa mfumo wa stakabadhghalani ambao unamlinda mkulima dhidi ya walanguzi wa mazao ya kahawa,ufuta,soya,mbaazi na korosho.

imeandikwa na Albano Midelo 


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.