• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIONGOZI wa Dini watahadharishwa utakatishaii fedha haramu

Imewekwa kuanzia tarehe: August 1st, 2024

MSAJIRI wa Jumuiya za Kiraia kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Imanuel Kihampa  amewatahadharisha viongozi wa dini kujiepusha na utakatishaji wa fedha haramu na kufadhili  vitendo vya ugaidi.

Kihampa ametoa tahadhari hiyo wakati anatoa semina ya viongozi wa dini  wa Mkoa wa Ruvuma iliyofanyika kwenye ukumbi wa sekondari ya Songea Girls mjini Songea.

“Kwa bahati mbaya baadhi ya viongozi wa dini nchini wameruhusu Taasisi zao kutumika kutakatisha fedha haramu ambapo wameruhusu  fedha chafu  na kuziingiza kwenye mzunguko halali wa kifedha za kibenki ili ionekane ni fedha halali’’,alisema.

Amesema kwa kutokujua au makusudi baadhi ya viongozi wa dini wametengeneza mianya ya Taasisi zao kuruhusu utakatishaji wa fedha haramu kufanyika na kwamba serikali ilikuwa haiwatilii mashaka viongozi wa dini kwa sababu serikali ina Imani  kubwa na viongozi wa dini.

Amesisitiza kuwa viongozi wa dini ni wadau muhimu katika maendeleo ambapo amesikitishwa na baadhi ya viongozi wa dini kuruhusu vitendo hivyo kufanyika kupitia Taasisi zao ambapo amesema vitendo hivyo vina waweka viongozi wa dini kwenye mazingira ambayo sio salama yatakayowaingiza kwenye mtego mbaya na kuliingiza Taifa kwenye matatizo .

Amesema watu wenye nia ovu wanawaona viongozi wa dini kama mawindo hivyo wanaweza kuwatumia kufanikisha malengo maovu kwa kutumia mianya iliyopo kwenye Taasisi za dini ikiwemo utakatishaji wa fedha haramu na kufadhili ugaidi.

Awali akizungumza wakati anafungua semina hiyo,Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Joel Mbewa  amesema serikali inatambua mchango wa Taasisi za dini katika kudumisha amani na utulivu nchini na kutoa huduma mbalimbali za kijamii zikiwemo huduma za elimu na afya.

Amesema serikali itaendelea kukuza ushirikiano na Taasisi za dini ili kuhakikisha kuwa jumuiya za kidini zinajiendesha kwa uhuru na kwa kuzingatia sheria,mila na desturi.

Hata hivyo Katibu Tawala huyo ametahadharisha kuwa nchini yetu imekumbwa na viashiria vya uvunjifu wa maadili ya kijamii na jumuiya nyingi kuonekana kuwa katika hatari ya kuweza kutumika katika kuwezesha makosa ya utakatishaji wa fedha haramu na ufadhili wa ugaidi.

Mbewa amewaeleza viongozi hao,mafunzo hayo yanawajengea uwezo wa kutambua namna ya kuendesha jumuiya zao kwa kuzingatia sheria hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji kazi  na kulinda raslimali za jumuiya na kutojiingiza katika makosa ya utakatishaji wa fedha  haramu,ufadhili wa ugaidi na biashara haramu za silaha za maangamizi.

Kwa upande wake Shehe wa Mkoa wa Ruvuma   Ramadhani Mwakilima ameishukuru Ofisi ya Msajiri wa Jumuiya za Kiraia kwa semina hiyo  ambayo imewaongezea maarifa na kuwajengea uwezo wa namna bora ya kuendesha  Taasisi za kidini.

Naye Mwakilishi wa Kanisa Katoliki Sr.Janeth Hyera   amesema semina hiyo imewakumbusha mambo mbalimbali yaliyopo kwenye Taasisi wanazozisimamia ambayo yamesababisha baadhi ya Taasisi za kidini kufungiwa kwa kutotekeleza sheria na miongozo ya serikali.

Amesisitiza kuwa hivi sasa mambo mengi yanayofanyika inawezekana baadhi ya viongozi wa dini wanachangia kuwepo kwa maovu hayo ikiwemo usafirishaji  haramu wa binadamu ambao unapoteza vijana wengi ambao wanadai wanapata fursa ya Kwenda kusoma nje ya nchi ambako wanatendewa mambo mengi ya kigaidi.

Naye Katibu wa Kamati ya Amani Mkoa wa Ruvuma Askofu  Elimu Mwenzegule  amesema mafunzo yamewashirikisha viongozi wa dini kutoka wilaya zote mkoani Ruvuma ambapo ameishauri serikali kuhakikisha semina muhimu kama hizo ziwe endelevu ili kuwajengea uwezo viongozi wa dini ambao wanawajibu mkubwa wa kudumisha amani na utulivu hapa nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.