• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VISIWA vitatu vinavyofungua fursa mpya za utalii Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: April 22nd, 2025

Na Albano Midelo 

Katika pembe ya kusini mwa Tanzania,Ziwa Nyasa Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma kuna hazina ya asili ambayo bado haijagunduliwa na wengi .

Visiwa vitatu vya Mbambabay, Lundo na Puulu,hivi si visiwa vya kawaida; ni visiwa vyenye hadithi, historia na mandhari ya kuvutia kiasi cha kuibua hisia na hamu ya kutaka kufahamu zaidi.


Mbambabay: Kisiwa cha Mapango na Samaki wa Mapambo

Kisiwa cha Mbambabay, kinachotajwa kuwa moja ya vivutio vya utalii wa kipekee, kimejaa mapango yanayotumika na wavuvi kama hifadhi salama wakati wa dhoruba kali. 


Ni mahali pa asili ambapo mazingira yanazungumza ,hewa safi, sauti za ndege, na mwonekano wa samaki wa mapambo wanaoangaza chini ya maji safi ya Ziwa Nyasa. 

Kwa wapenzi wa mazingira ya kuvutia na utulivu, kisiwa cha Mbambabay ni patanisho  na sehemu asili  inayovutia wengi.


Lundo: Historia Yenye Machungu na Mafundisho

Kisiwa cha Lundo kinabeba simulizi ya binadamu na jamii ,historia ya wagonjwa wa ukoma waliotengwa na kupelekwa kuishi kisiwani humo wakati wa utawala wa wajerumani 

Makaburi ya waliopoteza maisha yao kutokana na ugonjwa huo bado yapo, yakielezea namna jamii ya wakati huo ilivyokabiliana na hofu ya maradhi. 

Waliopoteza maisha walizikwa kwa kufunikwa na tope, imani ikisema hilo lingesaidia kutokomeza ugonjwa wa ukoma.

Lundo si tu kivutio cha kiasili, bali pia mahali pa kutafakari kuhusu historia, utu na maendeleo ya kijamii.


Puulu: Makazi ya Ndege wa Ajabu 

Kisiwa cha Puulu, kilichopo Kata ya Liuli, ni mahali panapopaswa kutembelewa na kila mpenda maajabu ya asili. 

Kisiwa hiki Kina mazalia ya samaki wa aina nyingi, wakiwemo wale wa mapambo. Lakini kivutio cha kipekee zaidi ni ndege maarufu duniani ajulikanaye kama ngwazi, anayejulikana kwa ustadi wake wa kipekee wa kuvua samaki kutoka majini. 

Visiwa hivi ni hazina ambayo inahitaji kuangaziwa zaidi, kutangazwa kitaifa na kimataifa, na kuwekewa miundombinu rafiki ili kuwavutia watalii wa ndani na wa kimataifa.

Wilaya ya Nyasa, kupitia vivutio hivi, inaweza kuwa kitovu kipya cha utalii endelevu kusini mwa Tanzania .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.