• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WACHIMBAJI wadogo Mbinga kusogezewa huduma za afya

Imewekwa kuanzia tarehe: November 29th, 2021

WACHIMBAJI wadogo wa dhahabu wanaofanya shughuli zao  katika kijiji cha Lukalasi kata ya Kigonsera wilayani Mbinga,wameiomba Serikali  kuwasogezea  Huduma za Afya kwa kujenga zahanati au kituo cha Afya ili waweze kupata  huduma za matibabu ikiwemo za kifua kikuu na chanjo ya Covid-19.

Wametoa maombi  hayo jana, wakati wa  zoezi la kampeni ya uibuaji na upimaji wa vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu(TB) kwenye machimbo inayofanywa na Hospitali ya Halmashauri ya wilaya Mbinga  na wataalam wa shirika la Management and Development for Heath(MDH).

Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji hao Elimwaria Muro alisema, katika eneo hilo kuna watu zaidi ya  elfu mbili wanaofanya kazi ya kutafuta na kuchimba  dhahabu lakini  hakuna huduma za afya.

Hivyo alisema, wakati umefika kwa Serikali kupitia wizara ya afya kuwajengea zahanati au kituo cha afya ili jamii inayoishi eneo hilo waweze kupata huduma za matibabu jirani na  makazi yao.

Kwa mujibu wa Muro,iwapo Serikali itasogeza huduma za afya katika eneo hilo jamii itakuwa na afya njema  na kuwawezesha kushiriki kazi mbalimbali za maendeleo na  kutoa mchango mkubwa kujenga uchumi wa nchi yao.

Aidha Muro ambaye ni Mhandisi wa mgodi wa dhahabu wa Lukalasi unaomilikiwa na mzawa Jonson Nchimbi, ameipongeza Serikali  kupitia wizara ya afya kupeleka huduma ya uchunguzi  wa ugonjwa wa kifua kikuu kwa kutumia cliniki inayotembea(Mobile Clinic) kwa wananchi waishio maeneo ya machimbo ya  madini.

Edwin Nchimbi alisema, kwa sasa wanalazimika kutembea umbali mrefu hadi kijiji cha Kigonsera au Mbinga mjini  kufuata matibabu,jambo ambalo ni kero  kubwa na linawapotezea muda mwingi wa kufanya kazi za maendeleo.



Naye Dkt Bingwa wa magonjwa ya ndani ya Binadamu Dkt Dennis Ngatenelela alisema,serikali imelazimika kutumia cliniki inayotembea kuwafikia wananchi wanaoishi maeneo ya pembezoni ili waweze kupata huduma mbalimbali za afya.



Alisema, mpango wa Serikali kupitia wizara ya afya ni kuhakikisha kila mtu anapata huduma  pale alipo na hakuna mwananchi atakayepoteza maisha kwa kukosa matibabu,ndiyo maana wamelazimika kupeleka huduma za uchunguzi hadi katika maeneo  hayo.


Akizungumzia ugonjwa wa kifua kikuu Dkt Dennis alisema, tafiti za kitaalam zinaonesha kuwa kuna uhusiano wa karibu kati ya shughuli za uchimbaji wa madini na ugonjwa wa kifua kikuu kutokana na vumbi linalotoka wakati wa kutafuta na kuchimba madini kuingia  ndani ya mwili wa Binadamu.



Alisema,wadudu wa kifua kikuu mara nyingi wanakaa katika miili ya binadamu na ugonjwa huo unatibika kwa mtu aliyeambukizwa kupata matibabu yanatolewa bure katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya.



Kwa upande wake mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga Dkt Bryson Mapunda alisema, matibabu ya kifua kikuu ni ya miezi sita na mgonjwa anatakiwa kunywa dawa kila siku bila kuacha.



Alisema, ni muhimu kumaliza dozi au matibabu kama ilivyoelekezwa na muhudumu wa afya na kuonya kuwa, kuacha kunywa dawa kikamilifu kuna weza kusababisha vimelea kuwa sugu na hivyo kuambukiza watu wengine.



Dkt Mapunda alisema, kifua kikuu sio ugonjwa wa kulogwa wala kurithi bali ni ugonjwa unaoambukizwa na vimelea aina ya bakteria visivyoonekana kwa macho bali kwa kutumia hadubini.


Amewashauri, watu wenye dalili za ugonjwa huo  kuwahi kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kwa ajili ya uchunguzi na kifua kikuu kinatibika na kupona kabisa hata kama ana mgonjwa maambukizi ya virusi vya ukimwi.


Alisema, mtu anapaswa kupata matibabu  mapema ili kuzuia maambukizi kwa wengine na mgonjwa ambaye ameanza tiba sio rahisi kuambukiza mtu mwingine,hivyo hakuna sababu ya kumtenga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.