• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFANYAKAZI 56 wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana Songea waanza mafunzo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2023

Na Albano Midelo,Songea

WAFANYAKAZI 56 wa vituo vya kulelea Watoto  wadogo mchana wilayani Songea mkoani Ruvuma wameanza mafunzo ya siku tano kwenye ukumbi wa Anglikana mjini Songea.

Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI na kusimamiwa na Idara ya Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma ambapo wawezeshaji wa mafunzo hayo ni Taasisi ya ANJITA ambayo imepewa Mamlaka ya kutoa mafunzo hayo.

Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo,Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma Victor Nyenza amesema katika Mkoa wa Ruvuma kuna vituo 138 vya  kulelea Watoto wadogo mchana na kwamba kati ya vituo hivyo ni vituo 68 tu ndiyo vimesajiriwa.

Ametoa rai kwa vituo ambavyo bado havijasajiriwa kuhakikisha wanavisajiri vituo vyao na kwamba ifikapo Januari 2024 vituo vyote viwe vimesajiriwa vinginevyo vitafungwa.

“Hatutarajii katika Mkoa wa Ruvuma kuwa na kituo cha kulelea Watoto mchana ambacho hakisajiriwa na  kina walezi wa Watoto wasiokuwa na sifa ya mafunzo elekezi kwa vitendo,vituo ambavyo vitakuwa havina sifa tutakwenda kuvifunga kwa mujibu wa sheria’’,alisisitiza Nyenza.

Amesisitiza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa walezi wa watoto kwa kuwa wanakwenda kupata mbinu na stadi mbalimbali za kuboresha na kuimarisha malezi ya Watoto wanaohudumiwa.

Amesisitiza kuwa vitendo vingi vya ukatili wa Watoto na  matukio mengi ya utekaji na utelekezaji wa Watoto yanafanyika pia kwenye vituo vya kulelea Watoto wadogo na kwamba Watoto wengi wanatekwa wakiwa katikati ya kituo cha malezi na nyumbani hivyo ameagiza kila kituo kiwe na rejesta ili kusaidia wamiliki wa vituo kujiweka upande salama.

Amelitaja  jukumu la walezi wa Watoto wadogo mchana kuwa ni kumwandalia mazingira wezeshi mtoto ili aweze kukua vizuri na kuelewa stadi tatu za kusoma,kuandika na kuhesabu.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo Mratibu wa mafunzo kutoka Taasisi ya ANJITA  Janeth Malela amezitaja mada  ambazo zitafundishwa kwenye mafunzo hayo kuwa ni sayansi ya dhana ya malezi ,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto uanzishaji na usimamizi wa vituo vya Watoto na vifaa vya kujifunzia na kuchezea Watoto.

Mada nyingine amezitaja kuwa ni mbinu za ujifunzaji na kuelewa Watoto kuanzia miezi sita hadi miaka sita,afya lishe na usafi wa mazingira,ulinzi na usalama kwa mtoto,utambuzi wa mapema na afua stahiki kwa Watoto wenye mahitaji maalum,namna ya kufanya tathmini ya maendeleo ya mtoto na mafunzo kwa vitendo.

Aliyesimama ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma Victor Nyenza akizungumza wakati anafungua mafunzo ya wanafanyakazi wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana kwenye ukumbi wa Kanisa Anglikana mjini Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.