• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFUGAJI Songea washauriwa kutumia teknolojia rahisi ya ufugaji kuku

Imewekwa kuanzia tarehe: December 10th, 2020

WAFUGAJI Songea washauriwa kutumia teknolojia rahisi ya ufugaji kuku

Wafugaji wa kuku wa Kijiji cha Nakahegwa  wilayani Songea mkoani Ruvuma wameshauriwa kutumia teknolojia rahisi katika kufanikisha malengo yao ya ufugaji ili waweze kupata mafanikio ambayo yatawawezesha kupunguza umasikini wa kipato katika kaya zao.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea  Dr Erick Kahise katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wafugaji kuku wa kikundi cha Federation Moja kilichopo katika kijiji hicho.

Dr Kahise amesema ili mfugaji  wa kuku aweze kupata mafanikio chanya afuate kanuni na taratibu za ufugaji kupitia teknolojia rahisi ikiwemo ujenzi wa mabanda ya kawaida ambayo vifaa vyake vinapatikana katika mazingira  wanayoishi.

Amewashauri wafugaji kuwashirikisha wataalam wa mifugo kuanzia hatua ya awali ya utayarishaji wa banda, matumizi ya chanjo na utengezaji wa chakula ambao unafaa kulisha kuku.

“Ufugaji usiozingatia kanuni na taratibu za ufugaji unasababisha hasara kwa wafugaji kufuatia kuku hasa vifaranga kukumbwa na magonjwa na vifo jambo linalorudisha  nyuma jitihada za kujinasua na umaskini wa mtu mmoja mmoja au kaya’’,alisisitiza Dr.Kahse.

Kwa upande wake Mlezi wa kikundi hicho Remigiusi Mbawala amesema kikundi hicho ni cha hiari ambacho kinamtaka kila mwanachama kutekeleza majukumu yake bila shuruti ili aweze kujipatia kipato chake kupitia mradi wa ufugaji kuku.

Naye Mratibu wa kikundi hicho Sponsa Dimayo amewaomba wataalam wa mifugo mara kwa mara kuwatembelea na kuwapa elimu na ushauri ambao utawabadilisha kimtazamo kuacha kufuga kuku  kwa mazoea na kuanza kufuga kuku kwa njia ya  kisasa.

Mratibu  Mfuko wa Wanawake kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Songea  Xveria Mlimira amewataka wanakikundi kutimiza vigezo vya kukopeshwa  ili waweze kukopeshwa mikopo inayotolewa na Halmashauri   hali itakayosababisha ufugaji kuwa endelevu.

Kikundi cha Fideration Moja  kilianzishwa mwaka 2016 kikiwa na jumla ya kina wanachama 12 ambao wanajishugurisha na shughuri ya ufugaji kuku na kilimo cha mazao ya bustani.

Imeandikwa na Albano Midelo

Desemba 10,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.