• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFUGAJI waliovamia hifadhi ya Taifa ya Nyerere kuondolewa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 24th, 2021

WAZIRI wa maliasili na utalii Dkt Damas Ndumbaro, ametangaza

operesheni kabambe ya kuwaondoa wafugaji wote waliovamia na kufanya

shughuli zao katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere na maeneo mbalimbali

yaliyotengwa kwa ajili ya utalii hapa nchini.

Dkt Ndumbaro ametangaza hatua hiyo jana wakati akiongea na wananchi wa

vijiji vya Kalulu na Jakika wilayani Tunduru, wakati wa ziara yake ya

kusikiliza kero ya wananchi kuhusiana na wanyamapori wanaovamia

mashamba na kufanya uharibifu wa  mazao wilayani  humo.

Alisema, tatizo la wanyama hususani Tembo wanaokula mazao ya wakulima

limechangiwa kwa kiasi kikubwa na wafugaji kuingiza mifugo yao kwenye

maeneo yasioruhusiwa kisheria jambo linalosababisha wanyama  hao

kukimbia.

Kwa mujibu wa Dkt Ndumbaro Serikali imeshatenga maeneo maalum kwa

ajili  ya shughuli za ufugaji, lakini kutokana na kiburi cha fedha

wafugaji  wanawatumia baadhi ya wenyeviti na watendaji wa serikali za

vijiji wasiokuwa waaminifu kukahidi na kupeleka mifugo  kwenye maeneo

waliyotengewa.

Dkt Ndumbaro amewaonya wenyeviti na watendaji wa vijiji hao kujiepusha

 na vitendo  vya rushwa kwa kupokea fedha na kuruhusu wafugaji kufanya

shughuli zao kwenye maeneo ya utalii kwani tabia hiyo ni  kukiuka

sheria za utumishi wa umma.

Waziri Ndumbaro, amewataka wananchi kuepuka  kuishi  kufanya shughuli

zao kwenye hifadhi kwani serikali  haitahusika kulipa fidia wala kutoa

kifuta machozi kwa mtu atakayepoteza maisha,kujeruhiwa na kuharibiwa

mazao.

Alisema, ili kukabiliana na wanyama wanaovamia mashamba na kuharibu

mazao,serikali kupitia wizara ya  maliasili imeanza kutoa mafunzo kwa

vijana kwenye vijiji vinavyozungukwa na hifadhi na mapori ya akiba ili

kuwajengea uwezo wa kufukuza wanyama pindi wanapofika kwenye makazi ya

watu.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro

alisema,wilaya  hiyo ni ya kilimo lakini changamoto kubwa   kuvamiwa

na wafugaji na mifugo mingi kutoka katika maeneo mengine ya nchi jambo

lililo sababisha kutokea kwa migogoro kati ya jamii ya wafugaji na

wakulima.

Alisema, licha ya serikali ya wilaya kutenga zaidi ya vitalu 200  vya

ufugaji,lakini jambo la kusikitisha baadhi ya viongozi wa ngazi za

vijiji wanaruhusu wafugaji kupeleka mifugo kwenye maeneo

yasioruhusiwa.

Mtatiro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama alisema,

katika kukabiliana na changamoto hiyo serikali ya wilaya inafanya

operesheni za mara kwa mara kuwaondoa wavamizi wote wanaofanya

shughuli za kibinadamu kwenye hifadhi na maeneo yote yasioruhusiwa.

Baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo,wameiomba serikali kupitia upya

viwango vya fedha vinavyotolewa kwa waathirika wa matukio ya

kushambuliwa na wanyama wakali  na  wanao haribu mazao kwani

havilingani na hasara inayotokea.

Mwenyekiti wa Baraza la wazee wilaya ya Tunduru Ajili Kalolo alisema,

wananchi wanalazimika kuondoa mazao yao mashambani kabla hayajakomaa

ili kuepuka kuliwa na wanyama.Kalolo alisema, kama serikali itaendelea na msimamo wake wa kuwaona

wananchi ndiyo wenye makosa kwa kile kinachodaiwa kuvamia kwenye

hifadhi basi kuna hatari wilaya hiyo kukumbwa na janga la njaa.

Msanga Rashid mkazi wa kijiji cha  Kalulu, ameiomba wizara ya

maliasili kuwasaidia kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu wa

mazao,badala ya kuwaona wananchi  ndiyo wakosaji kwani kama serikali

itaendelea na msimamo huo kuna hatari  baadhi ya vijiji kutokuwa na

watu kwa kuuawa na wanyama.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.