• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAGONJWA 496 Namtumbo wagundulika na shinikizo la juu la damu

Imewekwa kuanzia tarehe: July 19th, 2024

WATU  496 sawa na asilimia 71   kati ya watu  696 waliofanyiwa uchunguzi wa awali wa magonjwa ya moyo kutoka vijiji mbalimbali katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, wamebainika kusumbuliwa na shinikizo la juu ya  Damu.

Wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa chakula wenye uhusiano wa moja kwa moja na ugonjwa wa moyo ni asilimia 37na wagonjwa 222 sawa na asilimia 32 wamegundulika kuwa na matatizo ya kisukari.

Hayo yamesemwa  na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete(JKCI) Dkt Baraka Ndelwa,wakati wa zoezi la awali la uchunguzi wa magonjwa ya moyo na shinikizo la damu lililofanyika katika kijiji cha Luhimbalilo kata ya Mputa wilayani Namtumbo.

Amesema,wametoa rufaa kwa wagonjwa watano kwenda Hospitali ya Jakaya Kikwete kwa uchunguzi zaidi na wagonjwa wengine wamewapa rufaa  kwenda Hospitali ya Rufaa ya mkoa Songea (Homso)na Hospitali ya St Joseph Peramiho.


Dr. Ndelwa ameema,katika zoezi hilo wamegundua watu wengi wanaugua magonjwa ya moyo na sukari, lakini wanashindwa kupata matibabu ya uhakika kutokana na upatikanaji wa matibabu ya  kwenye ngazi ya zahanati na vituo vya afya kutokuwa rafiki.

Amesema,ugonjwa wa  shinikizo la damu husababisha matatizo mbalimbali ikiwemo kiharusi,na moyo kushindwa kufanya kazi hali inayoweza kusababisha kifo kwa mgonjwa ambaye hajapata matibabu.


Dkt Ndelwa,ameshauri kuanzishwa kliniki maalum za uchunguzi wa magonjwa ya moyo na shinikizo la damu  kwenye vituo vya afya na Hospitali za wilaya, ili kuweza kuwafuatilia kwa karibu wananchi watakaobainika kupata ugonjwa huo,na kuwawezesha watoa huduma vifaa vya kisasa vya kutolea huduma kwa wagonjwa.

Ameiomba serikali,kupeleka dawa za magonjwa ya moyo na kisukari kwenye zahanati  ili ziweze kuwasaidia wananchi wengi wenye matatizo hayo,badala ya kuishia kwenye Hospitali za rufaa za mkoa ambako upatikanaji wake ni rahisi.








Muuguzi kutoka Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete(JKCI) Silvia Millanzi alisema,watu wengi waliojitokeza kwenye kambi za uchunguzi na matibabu  katika kituo cha afya Lusewa,Hospitali ya wilaya Namtumbo na kituo cha afya Mputa wanafahamu hali za afya zao.





Hata hivyo,changamoto kubwa ni kutofuatilia matibabu kutokana na hali ya kiuchumi au upatikanaji wa dawa kwenye maeneo yao,jambo ambalo  ni hatari kwa sababu mgonjwa asiyepata matibabu  anaweza kupata magonjwa mengine hatari ikiwemo figo.





Millanzi,ameiomba jamii hasa watu wanaosumbuliwa na ugonjwa wa shikinikizo la damu,kuhakikisha wanazingatia maelekezo ya wataalam kuhusu  umuhimu wa kutumia dawa hizo kila siku katika maisha yao, ili kuzuia madhara zaidi yanayoweza kutokea.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.