• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAGONJWA wa kifua kikuu 1728 wagundulika Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: May 24th, 2022

HOSPITALI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, kupitia kitengo cha kifua kikuu na ukoma imefanikiwa kuibua wagonjwa 1,728 wenye maambukizi ya kifua kikuu kuanzia mwaka 2020 hadi Januari 2022.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dkt Wilfred Rwechungura, wakati akielezea mafanikio na mikakati ya kampeni ya kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu inayoendelea katika wilaya hiyo.
Dkt Rwechungura alisema,kuanzia mwaka 2020 Hospitali ya wilaya chini ya kitengo hicho imekuwa na mafanikio makubwa katika
mapambano dhidi ya ugonjwa wa TB kwani kila mwaka imekuwa inavuka malengo wanayopewa na Wizara ya Afya.

Alisema,mwaka 2020 waliwapewa malengo ya kuibua wagonjwa 647, lakini kutokana na mikakati waliyojiwekea na kutekeleza waliibua wagonjwa 709 wanaume 387 na wanawake 322.

Aidha alisema kati ya watu hao walioibuliwa,watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na tano ni 221,na watoto 105 walio chini ya miaka mitano walipata dawa kinga(IPT) na 171 wanaoishi kwenye familia za wagonjwa wa TB ya mapafu walichunguzwa.

Dkt Rwengura aliongeza kuwa,katika kipindi hicho watu waliopimwa virusi vya ukimwi walikuwa 709 ambapo 79 waligundulika kuwa na virusi vya ugonjwa huo na wote wameanzishiwa Dawa.

Kwa mujibu wa Dkt Rwechungura, mwaka 2021 malengo ilikuwa kuibua wagonjwa 741,hata hivyo walifanikiwa kuibua 768 kati yao wanaume 403 na wanawake 365 ambapo watoto walio chini ya miaka 15 walikuwa 289 huku waliopimwa VVU ni 768 na waliokutwa na maambukizi ni 55.

Alisema, mwaka huo 2021 familia za watoto walio chini ya miaka mitano wenye TB ya mapafu ambao walichunguzwa ni 221 na walioanzishiwa dawa kinga walikuwa 179 na watu 13 walipoteza maisha.

Pia alieleza,kwa mwaka 2022 wamepewa malengo ya kuibua wagonjwa 841,lakini katika robo ya tatu iliyoanzia Mwezi Januari hadi Machi,tayari wamefanikiwa kuibua jumla ya watu 251 kati yao wanaume 139 na wanawake 112.

Kwa mujibu wake,katika muda huo watoto walio chini ya umri wa miaka 15 waliogundulika kuwa na TB ni 77 na waliopima VVU walikuwa 251 ambapo watu 9 wamekutwa na maambukizi na wote wameanzishiwa Dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo .

Naye Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa wilaya hiyo Dkt Mkasange Kihongole alisema,katika malengo ya mwaka huu Hospitali ya wilaya imepewa lengo la kuibua wagonjwa 200,Hospitali ya Misheni Mbesa 150,Hospitali ya Kiuma 100,vituo vinavyopima makohozi Matemanga wagonjwa 15,Nakapanya 15,Mkasale 15,Mtina 15,Mchoteka 15 Zahanati ya Nandembo 10 na Namiungo wagonjwa 10.

Mkasange alieleza kuwa,katika miaka mitatu tangu kuanza kwa kampeni kabambe ya uelimishaji na uibuaji wa ugonjwa huo kumekuwa na mafanikio makubwa ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Alisema,mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano mkubwa wa watumishi wa idara ya afya kuanzia ngazi ya zahanati hadi wa Hospitali ya wilaya na wahudumu ngazi ya jamii.

Alisema, wahudumu ngazi ya jamii wamekuwa msaada mkubwa katika kampeni hizo kwa kuwa wanaokwenda kwenye mikusanyiko ya watu ikiwamo shule za bweni na maeneo mengine kwa ajili ya kutoa elimu ya kifua kikuu na kuchukua sampuli za makohozi na kupeleka Hospitali kwa ajili ya vipimo.

Aidha,amewashukuru wadau Shirika la MDH-Amref Heath Africa kwa mchango mkubwa wanaotoa wa kuwapa mafunzo wahudumu ngazi ya jamii na watumishi wa afya ambayo yamesaidia sana kuongeza morali ya utendaji na uwajibikaji.

Mkasange amevipongeza baadhi ya vyombo vya Habari ikiwamo Gazeti la Habarileo na Itv kwa mchango mkubwa, kwa kutoa elimu kwa jamii kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu.

Kwa mujibu wa Dkt Mkasange,ugonjwa wa TB unatibika kwa mtu aliyeambukizwa na mwenye dalili za ugonjwa huo kufika Hospitali kwa ajili ya uchunguzi na anayeabainika anaanzishiwa matibabu na kuacha mila potofu zinazohusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina.

Mkazi wa Tunduru aliyewahi kuugua ugonjwa wa kifua kikuu na kupoma Salome Golihama,ameishukuru serikali kuhamasisha jamii kujitokeza kwenye kampeni na elimu ya kifua kikuu kwa wananchi.

Alisema,hatua hiyo imesaidia sana jamii kufahamu dalili za ugonjwa huo na kujitokeza kwa hiari kupima na kuanza matumizi ya dawa ambazo zinatolewa bure.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.