• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAHUDUMU wa kujitolea Ruvuma wapewa msaada wa baiskeli 15

Imewekwa kuanzia tarehe: June 30th, 2021

WAHUDUMU  15 wa  kujitolea ngazi ya Jamii  ambao wamekuwa wanafanyakazi ya kuwasaidia watoto wa kaya masikini 423 mkoani Ruvuma wamepewa msaada wa baiskeli ili kuwasaidia kutoa huduma kwa jamii.

Msaada huo umetolewa na Shirika la Social Action Trust Fund(SATF) kwa udhamini wa mfuko wa dharura wa Rais wa Marekani wa kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI(PEPFAR), kupitia mfuko wa Balozi wa Marekani nchini Tanzania.

Akitoa taarifa kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Pololet Mgema katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea ,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa SATF Dkt.Sylivia Ruambo amesema jumla ya shilingi milioni 3.7 zimetumika kununua na kusafirisha baskeli hizo hadi Songea.

Dkt.Ruambo amebainisha kuwa SATF inatekeleza mradi wa tuwalinde watoto katika Halmashauri tatu za Mkoa wa Ruvuma ambazo amezitaja kuwa ni Madaba,Songea na Nyasa na kwamba mradi huo ni wa mwaka mmoja.

“Mradi umelenga kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu kupata huduma za elimu,afya,ulinzi na haki za mtoto pamoja na kuziwezesha kaya masikini  kujenga uwezo kiuchumi’’,alisisitiza Dkt.Ruambo.

Hata hivyo amesema,pamoja na shughuli nyingine,mradi huo uliwajengea uwezo wahudumu 15 wa kujitolea katika ngazi ya Kata ambao wamekuwa wanasaidia kuielimisha jamii kuhusu haki za mtoto na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Amesema,mradi umeamua kuwanunulia basikeli wahudumu hao ili kuwarahisishia usafiri na kuwafikia walengwa majumbani kwao.

Akizungumza baada ya kuwakabidhi basikeli hizo,Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Pololet Mgema ametoa rai kwa wahudumu hao kuzitunza basikeli hizo na kuendelea kuwatumikia walengwa kama mradi ulivyoelekeza.

“Natambua kazi yenu kwa sehemu kubwa ni ya kujitolea,hivyo nawaomba mtangulize  mbele maslahi ya jamii ili kuweza kutimiza adhima ya kuwahudumia’’,alisisitiza Mgema.

Mgema amelishukuru Shirika la SATF na PEPFAR kupitia ubalozi wa Marekani kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya mkoani Ruvuma ambako wanatekeleza mradi wa Tuwalinde ambao unahudumia watoto 423.

Naye Mwakilishi wa Balozi wa Marekani Jeremy Divis amesisitiza kuwa wapo tayari kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kutekeleza miradi mbalimbali yenye tija kwa jamii ukiwemo mradi wa tuwalinde ambao unatekelezwa pia mkoani Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 29,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.