• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAINGEREZA walivyoizamisha meli ya wajerumani bandari ya Liuli ziwa Nyasa mwaka 1914

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2024

Bandari ndogo ya Liuli mwambao wa ziwa Nyasa mkoa wa Ruvuma, inajulikana hasa kutokana hospitali ya Mtakatifu Anna ya kanisa Anglikana inayohudumia wagonjwa wengi katika wilaya   Nyasa.

Katika sekta ya utalii bandari ya Liuli ni eneo lenye utajiri wa vivutio vya utalii wa aina mbalimbali. Jina Liuli lina maana ya 'jiwe lile'. Wakati wa ukoloni wa Kijerumani Liuli iliitwa "SPHINXHAFEN" yaani bandari ya SFINKSI kwa sababu ya kuwepo utajiri wa miamba mikubwa inayofanana na sanamu mashuhuri kwenye Piramidi za giza kama nchini Misri.

Tarehe 13/8/1914 mwanzoni mwa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Waingereza walishambulia katika eneo la Liuli meli ya pekee ya Wajerumani kwenye ziwa Nyasa ambapo katika Jiwe kubwa la Pomonda lililopo meta 300 ndani ya ziwa Nyasa lilitumika kama maficho ya askari wakati wa vita.

Kwa mujibu wa habari katika gazeti la Times iliyochapishwa mwaka 1914, Uingereza iliwahi kuingia katika vita ya kwanza ya Dunia Agosti 4,1914 na kwamba Siku chache baadaye Nahodha Mwingereza Edmund Rhoades katika kisiwa cha Nkhata Bay nchini Malawi alipokea amri ya kuzamisha meli Hermann von Wissmann iliyokuwa meli  pekee ya Wajerumani kwenye ziwa   Nyasa.

Meli hii ilikuwa chini ya Nahodha wa kijerumani aliyeitwa Berndt ambapo baada ya kupata amri, Rhoades aliendesha meli yake HMS Gwendolyn kuelekea Sphinxhafen (Liuli) kwa sababu alijua meli ilikuwa wapi. Manahodha wote wawili walikuwa marafiki waliowahi kutembeleana mara kwa mara na kukaa pamoja.

HMS Gwendolyn ilipokaribia bandari ya Liuli, Mpiganaji mzinga wa pekee wa meli na mfanyabiashara mmoja Mskoti alikuwa mtu wa pekee mwenye kujua  matumizi ya mzinga hivyo alianza kufyatulia risasi dhidi ya Hermann von Wissmann.

Dakika chache baadaye boti ndogo ilikaribia haraka HMS Gwendolyn. Nahodha Berndt akapanda meli na kumwuliza mwenzake kwa hasira, kwa nini amelewa wakati wa mchana.

Hakujua kuwa vita ilianza tayari katika  bara la Ulaya hivyo  Rhoades  alimtangaza Nahodha wa kijerumani kuwa mfungwa wa vita.

Habari ya ushindi huo ilipelekwa London kwa simu na tarehe 16 Agosti mwaka 1914,gazeti la Times lilichapisha na kutangaza ushindi wa Uingereza katika bandari ya Liuli ziwa Nyasa "Naval victory on Lake Nyasa".

Wakati ule Waingereza waliondoa mzinga mdogo wa meli na vipuli kadhaa ili meli isitumike tena bila kuiharibu. Mwaka 1915 Wajerumani walikuwa wameleta tena vipuli na kutengeneza meli ambapo  Waingereza walirudi Liuli na kuzamisha meli ya Hermann von Wissmann katika bandari ya Liuli.

Baada ya vita meli ilifufuliwa tena na kufanya kazi kwa Waingereza ambapo hadi sasa  maboya yamewekwa katika eneo la Liuli kuonesha mahali  meli hiyo ilipozamishwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.