• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa kidijitali utakavyomlinda mkulima Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 3rd, 2024

Mradi wa AIDI TANZANIA umegawa mizani iliyounganishwa na mfumo wa simu  na vishikwambi ambayo itatumika kwenye vituo vya kukusanyia mazao  mkoani Ruvuma ili kuhakikisha  mkulima kupata kilo halali kwenye mazao yake.

Meneja wa mradi wa AIDI na Mkurugenzi wa Rotai Company Limited Felix Awino amesema hayo wakati anazungumza kwenye hafla fupi ya ugawaji wa vishikwambi na Mizani ya kieletroniki katika ukumbi wa Mipango uliopo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Awino amesema katika Mkoa wa Ruvuma  wanalenga kuingiza mazao ya mahindi maharage na Soya kwenye mfumo rasmi wa mauzo ya kidigitali na kwamba  ili mkulima atumie mzani itamlazimu awe amesajiliwa.

"Mradi wa AIDI upo  Kwa lengo la kuendeleza wakulima kwenye mfumo wa kijiditali na kwamba tumedhamiria kuhakikisha wakulima wadogo wanapata masoko ndani na nje ya nchi Kwa kupitia mifumo ya kidigitali", Amesema Awino.

Katika hafla hiyo wagani kazi 15 wamegawiwa vishikwambi ambapo AIDI imekusudia kuwafikia wagani kazi 300 waliopo Mkoani Ruvuma ambao watapata mafunzo ya namna ya kusajiri na kukusanya mazao Kwa njia ya kidigitali na mawasiliano ya anga.

Mgeni rasmi kwenye hafla hiyo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Jumanne Mwankhoo amezitaja faida za mfumo huu,  kuwa utasaidia wakulima kupata huduma za ugani katika sehemu ambazo hazina maafisa ugani kwa kuwa una upungufu wa maafisa ugani 600.

Amesisitiza kuwa Mradi huo utaongeza uhakika wa usalama wa chakula kutokana na kuongezeka Kwa tija katika uzalishaji na kwamba amewashauri maafisa ugani  waliopewa vifaa hivyo wavitunze na kuhakikisha vinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa BRITEN, Ainea Mgulambwa amesema wamejikita katika kuboresha mtandao wa usambazaji wa pembejeo ususani maeneo ya vijijini ili mkulima asipate shida ya kutembea umbali mrefu kufuata pembejeo.

Naye Afisa Mipango Soko la Bidhaa Tanzania, Eva Msangi ameitaja kazi kubwa ya  Taasisi yake ni  kukutanisha wauzaji na wanunuzi wa bidha Kwa kutumia mfumo wa kielectroniki na kuhakikisha ununuzi na ushindani wa bei katika masoko.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Afisa Udhibiti Ubora Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala ( WRRB) Witness Temba amesema kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghala wakulima na vyama vya ushirika vya msingi wanaweza kukusanya mazao yao katika maghala na wakapatiwa Stakabadhi  ambayo imebeba taarifa zote kuhusu mzigo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.