• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Ruvuma waingiza bilioni 644 baada ya kuuza kahawa na korosho

Imewekwa kuanzia tarehe: February 14th, 2023

Wakulima mkoani  Ruvuma waingiza zaidi ya shilingi bilioni 644 baada  kuuza mazao ya kahawa na korosho kwenye  misimu mitano mfululizo.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Mkoa wa Ruvuma kwa vipindi vya misimu ya kilimo mitano mfululizo kutoka msimu wa kilimo 2017/2018  hadi kufikia msimu 2020/2021 jumla ya kilo 77,664,927.75 za kahawa zilikusanywa.

Amesema kilo hizo  ziliuzwa kwa watani wa bei sh. 4,638 na kuwapatia wakulima  wa kahawa zaidi ya shilingi bilioni  353.

Amebainisha kuwa kati ya fedha hizo,msimu wa mwaka 2016/2017  zilinunuliwa kilo  15,393.500 zilizowaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni 66 na kwamba msimu wa 2017/2018 zilinunuliwa kilo 20,162,900 na kuwaingizia  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 74.

Kwa mujibu wa Kanali Thomas katika msimu wa mwaka 2018/2019 zilinunuliwa kilo 15,675,100 zilizowaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 64,msimu wa mwaka 2019/2022 zilinunuliwa kilo 12,676,844 zilizowaingiza wakulima zaidi ya shilingi bilioni 50  na kwamba mwaka 2020/2021  zilinunuliwa kilo 15,756,583.75 na kuwaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 97.

Akizungumzia kuhusu zao la korosho,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema kwa msimu wa masoko 2022/2023 minada ilianza tarehe 10/11/2022.

“Hadi kufikia tarehe 24/12/2022 Mkoa ulikusanya jumla ya kilo 6,123,688 za Korosho zenye thamani ya shilingi bilioni . 11,406,932,180 ambazo ziliuzwa kwa wastani wa bei sh. 1852.33 kwa kilo’’,alisema RC Thomas.

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma kwa vipindi vya misimu ya kilimo minne mfululizo kutoka msimu wa kilimo 2017/2018 hadi kufikia msimu 2020/2021 jumla ya kilo 104,819,739.00 za Korosho zilikusanywa na kuuzwa kwa wastani wa bei sh. 2,801 na kuwapatia wakulima  zaidi ya shilingi bilioni 291.

Amesema Serikali kupitia vyama vya Ushirika imetekeleza na inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi ikiwemo usimamizi wa uendelezaji wa ujenzi wa kiwanda cha vifungashio cha Chama Kikuu SONAMCU wilayani Namtumbo na ukarabati wa maghala matano kati ya saba ya Chama Kikuu cha Ushirika Mbinga MBIFACU.

Miradi mingine inayotekelezwa na ushirika ameitaja kuwa ni Ukarabati wa hoteli ya MBICU mjini Mbinga,usimamzi na uendelezaji wa Mradi wa kiuchumi wa shamba la kahawa  la MBIFACU,ujenzi wa Mradi wa shule ya Sekondari ya Mahenge AMCOS na Ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao ya wakulima la chama cha Msingi Kimuli na Namitili (AMCOS) wilayani Mbinga.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma katika msimu wa 2022/2023 unaendelea kutekeleza  mpango wa kilimo cha mazao kupitia kilimo cha pamoja (block Farming),ikiwa na lengo la kuongeza uzalishaji na kuweza kumpatia tija mkulima.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 14,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.