• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Ruvuma wauza kilo milioni 3.8 za ufuta kupitia mfumo wa TMX

Imewekwa kuanzia tarehe: June 5th, 2024

WAKULIMA mkoani Ruvuma wameuza jumla ya kilo milioni 3,836,889 za zao la ufuta kwa bei ya wastani wa shilingi 3,652.00 kwa kilo kupitia stakabadhi ya ghala kwa kutumia mfumo wa TMX.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed wakati anatoa salamu za Mkoa kwa Naibu Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi ambaye amefanya ziara ya kikazi ya siku moja wilayani Songea.

Amesema wakulima hao wameuza ufuta katika minada iliyofanyika katika wilaya za Namtumbo,Songea na Tunduru ambapo ameipongeza Wizara yenye dhamana ya teknolojia kwa kuwezesha utumiaji wa mfumo katika eneo la uuzaji wa mazao kwa njia ya stakabadhi za ghala.

Hata hivyo amesema wakulima mkoani Ruvuma msimu huu katika zao la mahindi wanatarajia kuvuna tani milioni 1,882,473 ,uzalishaji ambao umechangiwa kwa kiasi kikubwa na upatikanaji wa mbolea ya ruzuku.

“Mkoa  wetu hivi sasa unashika nafasi ya nne kitaifa kiuchumi,Pamoja na jitihada  za wananchi wetu ambao wanajishughulisha na shughuli za kilimo lakini uwekezaji uliofanywa katika makaa ya mawe unachangia Zaidi katika ukuaji wa uchumi katika Mkoa wetu’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Mkuu wa Mkoa ameyataja mafanikio mengine katika sekta za huduma za jamii ambapo katika sekta ya elimu,Mkoa umeweza kupokea wanafunzi wote wanaoanza kidato cha kwanza kwa mara moja.

katika eneo la afya  Kanali Abbas amesema Mkoa pia umepiga hatua kubwa ikiwemo ya kuwa na mashine ya kisasa ya CT-Scan jambo ambalo limerahisisha matibabu ya wagonjwa na kwamba mfumo wa matibabu umekuwa wa kidigitali.

Kuhusu Sekta ya umeme Kanali Abbas amesema,Mkoa umepata mafanikio makubwa ambapo vijiji 541 kati ya 554 vimeunganishwa na umeme sawa na asilimia 97.7

Akizungumzia eneo la sekta ya mawasiliano, amesema eneo kubwa la Mkoa wa Ruvuma lina mawasiliano ya simu na kwamba kuna maeneo machache ambayo hayana mawasiliano.

Kwa upande wake Meneja TTCL Mkoa wa Ruvuma Zabron Magabula amesema serikali inatarajia kujenga minara nane ya mawasiliano katika  Mkoa wa Ruvuma ambayo itaunganishwa na mkongo wa Taifa ili kupanua wigo na kuboresha mawasiliano ya intaneti na sauti.

Amesema ndani ya kipindi cha siku 50 serikali itajenga minara miwili ya mawasiliano katika vijiji vya Maposeni na Mdunduwaro wilayani Songea kwa gharama ya takribani shilingi milioni 600 ili kuboresha mawasiliano.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema serikali imedhamiria kusogeza huduma ya mawasiliano ya uhakika kwa wananchi kwa kuwa nchi inahitaji uchumi wa kidijitali.

Amesema serikali inaufanya Mkoa wa Ruvuma kuwa miongoni mwa mikoa inayokuwa katika teknolojia ya kidigitali ambapo amekagua maeneo ya Maposeni na Mdunduwaro ambako serikali imetoa fedha za kujenga minara miwili ya mawasiliano inayounganishwa na mkongo wa Taifa.

Naibu Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi akizungumza na wananchi wa Maposeni wilayani Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.