• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Tunduru waingiza bilioni 10.5 kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani

Imewekwa kuanzia tarehe: June 16th, 2023

Wakulima wa ufuta katika Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma wameingiza zaidi ya shilingi bilioni 10.5 baada ya kuuza tani 1626 za ufuta katika minada mitatu iliyofanyika kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani,

Hayo yamesemwa na Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Gorge Bisani katika mnada wa tatu wa ufuta uliofanyika katika kijiji cha Namiungo Tarafa ya Nakapanya ambapo wakulima waliridhia kuuza ufuta kilo shilingi 3,808,jumla ya kilo milioni moja na elfu sitini zimeuzwa.

Amesisitiza kuwa tani za ufuta zilizouzwa na wakulima katika minada mitatu iliyofanyika hadi sasa zinaweza kuvuka malengo ya kuzalisha ufuta kwa mwaka huu ambayo yalikuwa ni tani 3,000 hivyo uzalishaji unaweza kufikia zaidi ya tani 4,000 za ufuta kwa kuwa ufuta bado mwingi kwa wakulima.

Bisani amesema zao la ufuta linaonesha lina manufaa makubwa kwa wakulima na kuwa ni zao mbadala kwa korosho ambapo kwa mwaka huu bei ya ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani imekuwa kivutio kwa mkulima.

Ameyataja maeneo yanayoongoza kwa uzalishaji wa ufuta wilayani Tunduru kuwa ni Marumba, Lukumbule na Mtesa na kwamba zao la ufuta limebadilisha Maisha ya wakulima ambapo wakulima wengi wameweza kujenga nyumba za kisasa na kusomesha Watoto wao.

“Ukitaka kujua mchawi wa zao ni bei,bei inapokuwa nzuri sokoni inawashawishi wakulima kurudi shambani na kuongeza uzalishaji zaidi,naamini mwakani uzalishaji wa zao la ufuta utaongezeka maradufu’’,alisisitiza Bisani.


Naye Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU) Musa Manjaule akizungumza kwenye mnada wa tatu wa zao la ufuta uliofanyika katika Kijiji cha Nimiungo,alisema Katika mnada huo jumla ya Kampuni 11 zilishindanishwa ambapo kampuni saba zilifanikiwa kununua ufuta tani zaidi ya 1000 kwa bei ya wastani ya shilingi 3,808 kwa kilo.

Amesema bei ya ufuta ya shilingi 3,808 katika mnada wa tatu bado ni nzuri kwa wakulima wa Tunduru ukilinganisha na minada iliyofanyika katika mikoa ya Lindi na Songwe ambapo wakulima wameuza kilo  kwa shilingi 3,700.

Hata hivyo Manjaule ametoa rai kwa wanunuzi wa ufuta katika mnada ujao waendelee kuongeza bei ya ufuta kwa kuwa wakulima wanafanya kazi  katika mazingira magumu hivyo bei ya juu itatoa tija kwa mkulima kuongeza uzalishaji.

Rashidi Musa Mkulima wa ufuta katika Kijiji cha Namiungo akizungumza baada ya kufanyika mnada huo ameipongeza serikali kwa kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani,hata hivyo ameiomba serikali kukopesha wakulima dawa za kuongeza ubora wa ufuta.

Ally Omary Mkulima wa Namiungo amesema bei ya ufuta kwa mwaka huu,inatio moyo na kuwafanya wakulima ambao hawakulima mwaka huu,kujiandaa katika msimu ujao kulima ufuta kwa wingi.

Huu ni mnada wa tatu wa ufuta kufanyika katika wilaya ya Tunduru ambapo katika mnada wa kwanza uliofanyika AMCOS ya Lukumbule wakulima waliuza ufuta kilo shilingi 3,822 na katika mnada wa pili uliofanyika AMCOS ya Marumba wakulima waliuza ufuta kilo 3,895.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.