• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Tunduru wanavyojivunia mfumo wa stakabadhi ghalani

Imewekwa kuanzia tarehe: June 12th, 2023

WAKULIMA wa ufuta katika vijiji vya Moland na Lukumbule wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,wameingiza zaidi ya Sh.bilioni 6.4 baada ya kuuza kilo 1,626,991.70 katika minada mwili iliyofanyika kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika wilayani Tunduru(TAMCU Ltd)Iman Kalembo alisema,katika mnada wa kwanza uliofanyika kijiji cha Lukumbule wakulima waliuza kilo 857,977.70 zenye thamani ya Sh.bilioni 3,279,190.40. kwa bei ya Sh.3,822.

Alisema katika mnada wa pili uliofanyika katika kijiji cha Molandi kata ya Marumba, wakulima wamefanikiwa kuingiza sokoni kilo 769,014.00 zenye thamani ya Sh.bilioni 3,279,190,770.40 ambapo bei ilikuwa Sh.3,895.

Kalembo alieleza kuwa,katika msimu wa kilimo 2022/2023 lengo ilikuwa kuzalisha tani 350,000 sawa na kilo 3,500,000, lakini kutokana na mwitikio mkubwa wa wakulima katika uzalishaji wanaweza kuvuka malengo waliyojiwekea.

Amewaomba wanunuzi kuongeza bei ili kuwahamasisha wakulima waendelee na uzalishaji wa zao hilo ambalo linaonekana kuwa mkombozi mkubwa kiuchumi kwa wananchi wa wilaya ya Tunduru.

“bei zinapokuwa nzuri wakulima watahamasika kuzalisha kwa wingi zao la ufuta ambalo kwa sasa linaonekana kuwa mkombozi mkubwa kiuchumi kwa wananchi katika wilaya yetu”alisema Kalembo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tamcu Mussa Manjaule,amewataka wakulima wa kijiji cha Molandi kutumia muda wao katika shughuli za kilimo na kuuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ili waweze kupata bei nzuri na hivyo kujikwamua na umaskini.

Alisema,lengo la kujiunga katika vyama vya ushirika ni kutengeneza umoja utakaotetea maslahi ya wakulima na kuuza mazao kwa bei nzuri inayolingana na ghalama za uzalishaji badala ya kuuza kwa bei ya hasara au kupangiwa bei na wanunuzi.

Pia alisema,kupitia vyama vya ushirika wakulima watapata nafasi ya kujifunza namna mbalimbali ya kusimamia mazao yao ili yapate kuwa na thamani sokoni,matumizi sahihi ya fedha na kuirahisishia serikali kupata takwimu za uzalishaji na idadi ya wakulima wake wanaohitaji kupatiwa pembejeo.

Alisema,kijiji cha Molandi ni kati ya maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa ufuta na mazao mengine ya biashara ikiwemo korosho na mbaazi,kwa hiyo kama wataongeza juhudi kwa kupanua mashamba yao na kufanya kilimo chenye tija suala la umaskini katika kijiji hicho litakwisha.

Naye Afisa mazao wa wilaya ya Tunduru Gallus Makwisa,amewapongeza wakulima kwa kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalam wa kilimo ambayo yamesaidia sana kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara wilayani humo.

Alisema,maelekezo hayo yamekuwa chachu ya mafanikio makubwa katika sekta ya kilimo na kuwataka wakulima wa ufuta kuachana na kilimo cha mazoea na kufanya kilimo biashara ili waweze kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Aidha,amewataka kukumbuka kujiwekea akiba ya chakula kwa ajili ya mahitaji ya familia zao ili kuepuka kununua chakula kwa bei kubwa siku za usoni na kumshukuru Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro kwa kusimamia vizuri shughuli za kilimo na ushirika.

Baadhi ya wakulima,wameishukuru serikali kuendelea kusimamia soko la ufuta kwa mfumo wa stakabadhi ghalani,hata hivyo wameomba malipo yao yafanyike haraka ili fedha watakazolipwa zitumike kufanya maandalizi ya msimu mpya wa kilimo.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Ali Ngonji alisema,licha ya serikali kusisitiza suala la kuuza mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani,hata hivyo changamoto kubwa ni kucheleweshewa malipo hali inayochangia kukosa imani na mfumo huo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.