• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa kahawa Mbinga wanufaika na ruzuku ya pembejeo

Imewekwa kuanzia tarehe: March 14th, 2025

Wakulima wa kahawa katika Wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma, wameeleza kuridhishwa na mpango wa serikali wa kutoa pembejeo za ruzuku kwa misimu ya kilimo ya 2023/2024 na 2024/2025,Hatua iliyochangia kuongezeka kwa uzalishaji wa zao hilo. 

Kupungua kwa bei ya mbolea kumewawezesha wakulima kupata pembejeo kwa gharama nafuu, hali inayochochea maendeleo ya sekta hiyo. 

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Kahawa Mbinga (MBIFACU), Michael Kanduyu, amesema kuwa ruzuku hiyo imepunguza bei ya mbolea, ambapo UREA sasa inauzwa Sh. 68,000, CAN Sh. 62,000 na SA Sh. 48,000, ikilinganishwa na bei ya awali ya Sh. 150,000 hadi Sh. 180,000 kwa mfuko mmoja. 

Ameitaka serikali kupanua mpango huo kwa dawa za kupulizia kahawa ili kupunguza zaidi gharama za uzalishaji.

Lucas Mahay, mkulima kutoka Kijiji cha Malindindo, amesema kuwa kabla ya mpango wa ruzuku, wakulima walilazimika kupunguza ukubwa wa mashamba yao kutokana na gharama kubwa za pembejeo. Hata hivyo, mpango huu umewasaidia kurejesha matumaini na kupanua mashamba yao. Pia, amesifu hatua ya Mbifacu kuanzisha mfumo wa mikopo ya mbolea kwa wakulima, ambao umeongeza ushiriki wao katika vyama vya ushirika.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Mbifacu, Faraja Komba, amesema kuwa uzalishaji wa kahawa umeongezeka kutoka wastani wa tani 15,000 msimu wa 2021/2022 hadi tani 25,000 msimu wa 2024/2025. Ongezeko hilo limewanufaisha wakulima kwa mapato zaidi na kuchangia katika pato la serikali kupitia ushuru na tozo mbalimbali. 

Pia, vyama vya ushirika vimewekeza katika miradi ya maendeleo kama mashamba, vyombo vya usafiri na maghala ya kuhifadhi kahawa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.