• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa Kahawa Nyasa wazalisha miche ya kahawa zaidi ya 260,000

Imewekwa kuanzia tarehe: January 30th, 2020

Wakulima wa zao la kahawa Wilayani Nyasa, kwa kushirikiana na Vyama vya Msingi vya mazao na watu binafsi, wamezalisha miche ya kahawa 262,500 kwa msimu wa kilimo 2019/2020 ili kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa na kukuza uchumi  wa wananchi.

hayo yamesemwa na wakulima wa zao la kahawa katika Risala yao, kwa mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela O.Chilumba, wakati akizindua ugawaji wa miche mipya  ya kahawa aina ya “Compact” Uzinduzi uliofanyika  Hivi karibuni, katika Kijiji cha Kingerikiti Kata ya Kingerikiti Wilayani hapa.

Wakulima hao wamefafanua kuwa, wamelazimika kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa ikiwa ni pamoja, na utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Cassim Majaliwa aliyezitaka kili Halmashauri Nchini kuzalisha miche ya kahawa zaidi ya laki mbili.

Waliongeza kuwa Vyama saba vya Ushirika wa mazao vimezalisha miche hiyo na tayari kwa kugawa kwa wananchi kwa mchanganganuo ufuatao Nambawala AMCOS (10250), Kingerikiti AMCOS miche( 37,705), Tingi AMCOS (4,300) LIPO AMCOS MICHE (40,000), Mapendo AMCOS Miche (36,000) na Luhangarasi AMCOS 9890.

Pia wakulima hao walikipongeza kituo cha utafiti cha Ugano (TACRI) kwa kuwagawia bure miche kahawa 18,200 aina ya  compact, ambayo wameigawa kwa wakulima  ambao wanauhitaji wa miche hiyo.

Akitoa maelekezo ya upandaji wa miche hiyo kwa wakulima wa zao la kahawa, Ofisa kilimo wa Kata ya Kingerikiti ambaye pia ni Mkaguzi wa zao la Kahawa Bw.Richard Katale, aliwataka wakulima, kulihudumia vizuri, kwa kupanda kwa nafasi ya Meta mbili na kwa Hekari moja watapanda meche mia sita.

Aliongeza kuwa sifa za mche wa compact unazaa mapema na unavumilia ukame. Alikawataka wananchi  kupanda kwa maelekezo aliyoyatoa, ili kufikia uzalishaji wenye tija kwa kuwa Serikali imedhamiria kuboresha maisha ya wakulima wa zao la Kahawa.

Aidha wakulima hao, waliipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa kufanya maboresho mbalimbali ya zao la kahawa, na kuwaletea mnada wa kahawa katika Wilaya ya Mbinga na kuwapunguzia usumbufu kwa kuwa awali walikuwa wakienda moshi kufanyia mnada.

“kwa kweli awamu hii tunaona jinsi gani Serikali inatujali wakulima, kwa kuwa tunapewa mafunzo ya kulima kahawa, lakini pia kitendo cha kutupa miche ya ya kahawa bure , Serikali imetusaidia sana. Nimejaribu kupanda na nimeona ni mbegu nzuri inayotoa mavuno mengi kwa muda mfupi ukilinganisha na kahawa tuliyozoea kupanda awali”. Alisema Bonus mapunda mkulima wa zao la kahawa kutoka katika kijijii cha kingerikiti.

Akizungumza na wakulima wa zao la Kahawa Wilayani hapa, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Bw.Menance Ndomba aliyemwakilisha mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi,Isabela Chilumba,Aliwapongeza wakulima wa Zao la kahawa Wilayani Nyasa, kwa juhudi wanazozifanya za kulima na kutunza zao hilo na kuinua mapato ya Halmashauri na kuwa na kipato bora cha Familia na kuchangia maendeleo mbalimbali katika maeneo yao.

Aidha aliwataka kuendelea kuongeza uzalishaji wa zao la Kahawa kwa kuwa , Wilaya ya Nyasa ina Fursa ya  mashamba makubwa, kwa mujibu wa Utafiti uliofanyika hivi karibuni na “CAFE Afrika” katika Wilaya ya Mbinga na Nyasa Wilaya ya Nyasa ina fursa kubwa ya kupanua mashamba ya kahawa ukilinganisha na  Wilaya ya Mbinga.

“nachukua fursa hii kuwapongeza sana wakulima wa zao la kahawa Wilayani Nyasa, kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kujituma kulima na kuzalisha zao hili la kahawa ambalo linatupa faida kubwa sana katika Halmashauri yetu kama vile ,mapato ya ndani na mnachangia maendeleo mbalimbali katika maeneo yenu.Serikali ipo pamoja nanyi na itatatua changamoto mbalimbali mtakazokutana nazo katika shughuli zenu na kuhakikisha Miundombinu inajengwa. Alisema ndomba.

Wilaya ya Nyasa ipo katika Mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara ya Kahawa,kakao, na korosho ili kukuza uchumi wa kipato cha mwananchi mmoja mmoja na Wilaya kwa ujumla.

Imeandaliwa na

Netho c. Sichali

Ofisa Habari

Wilaya ya Nyasa 0767417597

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.