• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa kahawa washauriwa kutumia miche bora ya kahawa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 8th, 2020

Wakulima wa Mkoa wa RUVUMA wametakiwa kuchangamkia fursa ya kilimo cha kahawa kwasababu maeneo mengi ndani ya Mkoa yanafaa kwa kilimo cha kahawa ambacho kitainua uchumi wao.

Wito huo umetolewa na mtaalam wa kilimo Bw Victa Akulumuka kutoka kituo cha utafiti wa zao la kahawa TaCRI cha Ugano Mbinga katika maonesho ya nanenane ngazi ya Mkoa wa Ruvuma yanayofanyika viwanja wa Msamala mjini Songea.

Akalumuka amesema wakulima wanatakiwa kuchangamkia fursa ya kulima zao la kahawa kwakuwa zao la kahawa linaonekana kustawi katika maeneo mengi ndani ya mkoa na kilimo ambacho kitainua uchumumi wao na Taifa.

Amewataka wakulima kuzingatia amri kumi za kilimo cha kahawa ambazo zinasaidia katika kustawisha zao la kahawa ambazo zitatoa matokeo chanya na kuongeza uzalishaji wenye tija kwa wakulima .

Amezitaja amri za kilimo bora cha kahawa kuwa ni  kukatia matawi,kutumia mbolea,kupulizia madawa kwa wakati,kupalilia nakuondoa machipukizi Pamoja na kupanda miti kwa ajili ya kutunza ubaridi katika shamba.

Aidha amesema endapo wakulima watafuatilia na kusimamia na kufuatilia kilimo cha kahawa mkulima anaweza kuvuna kilo tatu kwa shina moja,ambapo kwa hekali moja mkulima anaweza kuvuna kilo Zaidi ya 1500 kutokana na shamba lenye ukubwa wa hekali moja ambapo hupandwa  miche 540

Ameomba maafisa ugani wa wa Halmashauri mkoani Ruvuma kutoa elimu juu ya usimamizi na ufuatiliaji wa zao la kahawa kwalengo la kuwasaidia wakulima kupata mavuno mengi na kunufaika na kilimo cha kahawa ambacho ni miongoni mwa mazao ya kimkakati Nchini.

“Ukichukulia miaka 10 iliyopita eneo la Liganga wilayani Songea kwenye shamba la kahawa la AVIV palikuwa hapajulikani kama panafaa kulima zao la kahawa lakini kampuni ya AVIV imeonesha mfano kwamba ardhi ya Ruvuma inafaa kwa kilimo cha kahawa”,alisema Akalumuka.

Utafiti umebaini kuwa mkoa wa Ruvuma  una maeneo mengi ambayo yanafaa kwa kilimo cha zao la kahawa ikiwemo Wilaya Mbinga na wilaya ya  Songea katika kata za Liganga,Mbingamhalule,Kizuka,Parangu LItisha,Ndongosi na Mpitimbi na Madaba.

Kituo cha utafiti wa zao la kahawa TaCRI kinatoa huduma ya miche bure kwa wakulima wote na utaalama wa kulima zao la kahawa unapatika kutoka kwa maafisa ugani.

Imeandikwa  na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Agosti 8,2020  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.