• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA watano na AMCOS moja Namtumbo washinda fedha na pikipiki za NMB

Imewekwa kuanzia tarehe: June 10th, 2023

BENKI ya NMB imezindua kampeni ya Bonge la Mpango Mchongo wa kilimo katika Kanda ya Kusini ambapo wakulima watano na Chama kimoja cha Ushirika cha Msingi (AMCOS) wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wameshinda.

Uzinduzi huo katika Kanda ya Kusini ulifanyika jana katika soko kuu la mjini Namtumbo mkoani Ruvuma ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya aliyewakilishwa na Msyangi Kuruchumila.

Mwakilishi wa Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Roman Degeleki aliwataja wakulima watano walioshinda shilingi 100,000 kila mmoja kwenye droo ya wiki hii katika kampeni hiyo kuwa ni  Alex Nombo wa Litembo Mbinga,Melina Saanze wa Mtwara,Malongo James wa Songea,Mustapha Milanzi wa Nanyumbu Mtwara na Hamidu Omary wa Mtwara.

Alikitaja Chama cha Msingi cha Ushirika (AMCOS) ambacho kimejinyakulia pikipiki kwenye mchongo wa kilimo kuwa ni Rwinga AMCOS ya mjini Namtumbo mkoani Ruvuma.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo,Meneja huyo wa Kanda alisema NMB imeamua kuzindua kampeni kabambe ya bonge la mpango mchongo wa kilimo awamu ya pili katika kanda ya kusini,ambapo AMCOS na wakulima watakaoweka akiba kupitia akaunti zao za NMB wataingia kwenye orodha ya wanaostahili kujishindia fedha taslimu,pikipiki za miguu miwili na miguu mitatu.

“Kwenye kampeni hii zaidi ya shilingi milioni 40 zitatolewa kama zawadi kwa washindi zaidi ya 50,kampeni itaendeshwa ndani ya wiki tano,kila wiki wakulima watano watapokea shilingi 100,000 kila mmoja na AMCOS moja itajinyakulia pikipiki’’,alisisitiza.

Kwa upande wake mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya ameupongeza uongozi wa NMB kwa kuamua kuleta kampeni ya Bonge la Mpango mchongo wa kilimo katika wilaya ya Namtumbo yenye wakulima wengi wanaozalisha mazao mbalimbali kama vile mahindi,ufuta,soya,korosho na mpunga.

Malenya ametoa rai kwa wakulima wa Namtumbo kuchangamkia fursa waliopewa na NMB kwa kuweka akiba na kufungua akaunti mpya ili kuanza kuweka akiba na kujishindia zawadi mbalimbali kutoka NMB.

“Ndugu zetu wa NMB wameenda hatua kubwa zaidi mbele,akiba unaweka kwa ajili yako,inabaki kuwa fedha yako,lakini wao wanakupa zawadi kwa kuwa umeamua kufungua akaunti na kuweka akiba,hili ni jambo kubwa sana,NMB wanastahili pongezi’’,alisisitiza Malenya.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa funguo za pikipiki kwenye uznduzi huo, kiongozi wa AMCOS ya Rwinga Mohamed Komba aliwapongeza NMB kwa kutoa zawadi ya pikipiki katika AMCOS hiyo baada ya kushinda ambapo alisema itawarahishia  kuwatembelea na kuwafikia wakulima kwa urahisi hivyo kuongeza tija kwenye kilimo.

Naye Rashid Abdalah Mkulima wa Namtumbo ametoa rai kwa Benki ya NMB  kutoa mikopo ya aina mbalimbali yenye riba nafuu kwa wakulima ili waweze kuzalisha kwa tija.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.