• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WALIOPEWA maeneo ya uwekezaji katika hifadhi watakiwa kuyaendeleza

Imewekwa kuanzia tarehe: October 1st, 2024

Na Gustaph Swai -Rs Ruvuma

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi, Dkt. Pindi Chana amewataka wawekezaji waliopewa maeneo katika maeneo ya uhifadhi kuwekeza na kuyaendeleza vinginevyo taratibu za kisheria zitachukuliwa.

Ameyasema hayo alipotembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimkakati katika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere Mkoani Ruvuma.

"Kuna watu wameshikilia maeneo katika maeneo yetu ya Uhifadhi, hakuna mtu anaendeleza, hapo unakosesha ajira kwa vijana, Mapato kwa Serikali, hilo hatutaruhusu, Wale waliopewa maeneo katika hifadhi wawekeze lasivyo taratibu za kisheria zitachukuliwa", Alisema.

Akiwa katika ziara hiyo, Balozi Chana amekagua lango la Kitalii la kisasa lakuingilia hifadhini hapo, Mradi wa ujenzi wa kiwanja cha Ndege, Nyumba ya wageni na  Ujenzi wa Nyumba za watumishi.

Sanjari na hayo, amebainisha kuwa Nchi ya Tanzania ina vivutio vingi vya Utalii na maeneo ya Wanyama ambapo shughuli mbalimbali za Utalii kama vile Utalii wa  uwindaji, upigaji picha na Utalii wa maji.

Ameeleza kuwa Wizara na Jeshi la Uhifadhi  limejipanga kuhakikisha rasilimali za Nchi zinalindwa  na ametoa rai kwa Wananchi kufuata sheria, kuacha kuchoma moto na kuingiza Mifugo katika Hifadhi.

Kwa Upande wake Kamishna Msaidizi Uhifadhi, Hifadhi ya Taifa ya Nyerere Ephraim Mwangomo amesema ujenzi wa Miundombinu ya hifadhi hiyo ikiwemo lango la kisasa, uwanja wa ndege na Nyumba za watumishi umegharimu Tsh. Bilioni 2.1.

Amewaomba wawekezaji kuja kuwekeza katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere akieleza kuwepo kwa idadi kubwa ya watalii wanaotoa fursa kwa wawekezaji hususani katika eneo la ujenzi wa Nyumba za wageni.

Sekta ya Maliasili na Utalii inachangia pato la Taifa kwa asilimia 17.5 na fedha za kigeni kwa asilimia 25

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.