• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANAFUNZI sekondari ya Mataka Tunduru waiomba serikali kukamilisha ujenzi wa bwalo

Imewekwa kuanzia tarehe: June 2nd, 2023

WANAFUNZI wa shule ya Sekondari Mataka kata ya Mchangani katika Halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,wameiomba serikali kukamilisha  haraka ujenzi wa bweni ili kuwaondolea kero ya kulala katika vyumba vya madarasa ya shule ya msingi Mataka.

Wakizungumza mbele ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Hairu Musa wamesema,kuendelea kulala kwenye madarasa inawasababishia kukosa muda wa kujisomea hasa nyakati za usiku kutokana na kuwepo kwa matukio ya wizi yanayofanywa na vijana kutoka mtaani.

Omari Rashid wa kidato cha tano amesema, kukosekana kwa ulinzi kunapelekea  kutumia muda mwingi kujilinda na kulinda vifaa vyao kama hatua ya kukabiliana na matukio hayo yanayotokea mara kwa mara.

Orestus Masoud amesema,matukio ya wizi yanayofanywa na watu wasiofahamika yanawanyima nafasi ya kuzingatia yale yanayofundishwa na walimu kwa sababu wanajikuta wanasinzia wakiwa  darasani.

Amesema,hali hiyo inatokana na muda wa usiku wanaotakiwa kupumzika kujilinda na waharifu hao wanaotoka katika maeneo mbalimbali ya mji wa Tunduru na kuiomba serikali kuongeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa uzio kuzunguka eneo lote la shule.

Mkuu wa shule hiyo Niver Mbunda amesema,wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kwa kushirikiana na Diwani wa kata ya Mchangani Hairu Musa wamechanga Sh.milioni nne kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bweni  lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 80.

Aidha amesema,Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini  Hassan Kungu katika kuunga mkono jitihada za wazazi kupitia mfuko wa Jimbo amechangia mifuko 600 ya saruji ambayo imesaidia kukamilisha boma na mwezi April mwaka huu Serikali imetoa Sh.milioni 80  ili kukamilisha ujenzi huo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mchangani Hairu Musa amesema,lengo la kujenga bweni hilo ni kuwezesha wanafunzi wa kidato cha tano na sita kuwa na sehemu nzuri na salama ya kuishi  na kuwaondolea changamoto ya kukaa kwenye madarasa ya shule ya msingi ambayo hayana ubora.

Hairu ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Tunduru amesema,wanahitaji zaidi ya Sh.milioni 130 kukamilisha kazi hiyo na kuiomba Serikali na wadau wengine kuendelea kuwaunga mkono kwa kuchangia fedha na vifaa vitakavyotumika kukamilisha ujenzi wa bweni na kujenga uzio kuzunguka eneo lote la shule.

Ameeleza kuwa,Halmashauri ya wilaya Tunduru kwa kushirikiana na wazazi,jamii na wadau mbalimbali wameanza kutekeleza mpango wa ujenzi wa mabweni katika shule zote za sekondari  kwa ajili kuwawezesha wanafunzi kuishi  shuleni ili wapate muda mwingi zaidi wa kujisomea hasa nyakati za usiku hatua ambayo itasaidia sana kuinua kiwango cha taaluma katika wilaya hiyo kongwe hapa nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.