• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI 900 Peramiho wapewa huduma za saratani

Imewekwa kuanzia tarehe: April 19th, 2025

Zaidi ya wananchi 900 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani bila malipo katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph Peramiho, mkoani Ruvuma, kupitia kambi maalum ya siku nne iliyohusisha madaktari bingwa kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Akizungumza wakati wa ziara yake hospitalini hapo, Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema kambi hiyo inalenga kutoa huduma za uchunguzi wa saratani ya matiti, tezi dume na aina nyingine, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kupambana na ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza.

“Takwimu zinaonesha watu 18 wamekutwa na viashiria vya saratani; kati yao wanawake 12 tayari wameanza matibabu na wanaume sita wamepewa rufaa kwa ajili ya uchunguzi zaidi,” amesema Waziri Mhagama na kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha huduma hizo muhimu kwa wananchi.

Ameongeza kuwa utafiti wa Tume ya Saratani (Oncology Commission Report) unaonesha kuwa ifikapo mwaka 2030, idadi ya vifo vitokanavyo na saratani katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara inaweza kuongezeka hadi kufikia watu milioni moja iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa.

Akitaja aina za saratani zinazoongoza hapa nchini, Mhagama amesema kuanzia mwaka 2019 hadi 2024, saratani ya mlango wa kizazi inaongoza kwa asilimia 41, ikifuatiwa na saratani ya matiti kwa asilimia 19, utumbo mkubwa na mdogo asilimia 6.1, koo asilimia 5.7 na saratani ya kichwa na shingo kwa asilimia 4.3.

Amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kuzingatia ulaji bora, kuepuka vyakula vyenye mafuta, chumvi,sukari nyingi, kuacha matumizi ya vilevi, na kupima afya zao mara kwa mara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo amesema taasisi hiyo imeamua kuwachukua wataalamu wanne kutoka Peramiho kwa ajili ya mafunzo maalum, ili waweze kutoa huduma za saratani kwa ufanisi zaidi pindi watakaporejea hospitalini hapo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.