• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Kata ya Kagugu Mbinga wakamilisha ujenzi wa zahanati

Imewekwa kuanzia tarehe: February 25th, 2023

WAKAZI  wa kijiji cha Makatani kata ya Kagugu Halmashauri ya Mji Mbinga mkoani Ruvuma,wanatarajia kuondokana na adha ya kutembea umbali  wa zaidi ya kilomita 25 kila siku kwenda kata jirani ya Tingi kufuata huduma za afya.

Wakazi hao wamepata matumani mapya baada ofisi ya Mkurugenzi wa mji Mbinga kuingilia kati na kuanza kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho iliyoanza kujengwa  zaidi ya miaka 17 bila kukamilika.

Diwani wa kata ya Kagugu Batson Mpogolo amesema, zahanati hiyo ilianza kujengwa mwaka 2006 kwa nguvu za wananchi lakini ujenzi wake ulisimama  kutokana na kukosa fedha za kukamilisha ili huduma ziweze kutolewa.

Mpogolo ameishukuru Halmashauri ya Mji Mbinga kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha kazi ya ujenzi wa zahanati hiyo ambayo imekamilika kwa asilimia 95.

Kwa mujibu wa Mpogolo, kazi zilizobaki  katika ujenzi huo ni kuchimba matundo ya vyoo na kujenga kichomea taka na kuwaomba wananchi wa kata hiyo kuendelea kuvuta subira wakati huu ambao serikali iko hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo.

Hata hivyo,ameiomba serikali kuharakisha kwa kuleta vifaa tiba na wahudumu ili zahanati iweze kuhudumia wananchi ambao bado wanaendelea kuteseka kwa kwenda maeneo mengine kufuata huduma za afya.

Mtendaji kata wa Kagugu John Makoyole amesema,kata ya Kagugu  yenye zaidi ya wakazi 1,820 kuna zahanati moja tu ya Makatani ambayo bado haijaanza kufanya kazi,hivyo wananchi wanalazimika kwenda kata nyingine kufuata huduma.

Amesema,hali hiyo imesababisha wananchi wengi kuwa maskini kwa kuwa wanakosa muda wa kufanya kazi za maendeleo,badala yake wanatumia muda mwingi kwenda maeneo mengine kufuata huduma za afya.Ameishuru serikali kwa uamuzi wake wa kumalizia kazi ya ujenzi wa zahanati hiyo ili wananchi wapate huduma za afya karibu na maeneo.

Aidha,ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuboresha baadhi ya huduma za kijamii ikiwamo maji,barabara na nishati ya umeme ambapo kati ya vijiji vitano vya kata hiyo,vitatu vimefikiwa na umeme.

Eliza Mapunda  mkazi wa kijiji hicho amesema,kukamilika kwa zahanati kutawezesha kuanza kutumika na kupunguza gharama walizokuwa wakitumia kusafiri  kwenda mbali kufuata huduma za afya  zinazopatikana kata za jirani na Hospitali ya wilaya Mbinga mjini.

Amesema,kwa sasa wanalazimika kutumia gharama kubwa kati ya shilingi 10,000 hadi 15,000 kwa usafiri wa boda boda kwenda kata ya Tingi kupata matibabu jambo lililowatesa kwa muda mrefu.

Mkazi mwingine Mathias Sangana amesema, kukamilika kwa zahanati hiyo italeta hamasa kubwa kwa akina mama wajawazito kuanza kliniki mapema na kujifungulia Hospitali kuliko sasa ambapo wajawazito wengi wanachelewa kuhudhuria kliniki mapema kutokana na gharama kubwa ya usafiri.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Mbinga Dkt Maximo Magehema amesema,serikali kupitia Halmashauri yam ji Mbinga iko hatua ya mwisho kukamilisha ujenzi wake.

Amesema,mara baada ya kazi za ujenzi zitakapokamilika itapeleka vifaa tib ana watumishi ili iweze kuanza kutoa huduma kwa wananchi wa kijiji cha Makatani na kata nzima ya Kagugu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.