• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Kipika Mbinga waiomba serikali kukamilisha mradi wa zahanati

Imewekwa kuanzia tarehe: March 1st, 2023

BAADHI ya Wananchi wa mtaa wa Kipika kata ya Matarawe Halmashauri ya mji Mbinga mkoani Ruvuma,wameiomba serikali kukamilisha haraka ujenzi wa zahanati yao ili waweze kuondokana na adha wanayoipata ya kufuata matibabu mbali na makazi yao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema, kwa sasa ujenzi wa zahanati hiyo umesimama kutokana na kukosekana kwa fedha, hivyo wameiomba serikali kutafuta mbinu mbadala ambazo zitawezesha kukamilika kwa ujenzi huo.

Amina Pili amesema,kwa muda muda mrefu wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya na wakati mwingine akina mama wajawazito wanajifungulia njiani wakati wakifuata  huduma na kuingia gharama kubwa ya usafiri hasa nyakati za usiku.

Amesema,wananchi wa mtaa huo kwa kiasi kikubwa wanategemea kupata huduma katika Hospitali ya wilaya Mbuyula pekee  iliyopo umbali wa km 5 na hakuna njia mbadala,jambo linalo sababisha baadhi yao kushindwa kuwahi katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa wakati na hivyo kupoteza maisha yao.

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa KipikaThomas Mahundi,ameipongeza Halmashauri ya mji Mbinga kuona umuhimu wa kupeleka ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itamaliza kero na usumbufu kwa wananchi wa mtaa wa Kipika na kata ya Matarawe kwenda maeneo mengine kufuata huduma za afya.

Amesema,zahanati hiyo itakapokamilika itawezesha na kusaidia kupunguza foleni  ya wagonjwa katika Hospitali ya wilaya Mbinga,na kuiomba serikali kufanya haraka kukamilisha zahanati hiyo ambayo itakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya mji Mbinga Dkt Maximo Magehema amesema, ujenzi wa zahanati hiyo umefikia asilimia 98 na gharama za ujenzi wake ni Sh.milioni 93 kati ya hizo shilingi milioni 62 zimeshatumika.

Dkt Magehema amesema,zahanati hiyo itakapokamilika itasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya mji Mbinga na kusaidia kusogeza huduma za afya kwa wananchi wa kata ya Matarawe.

Ameeleza kuwa,zahanati hiyo itawezesha wananchi kupata huduma karibu na makazi yao na watoto wadogo kupata huduma  muhimu za chanjo,badala ya wazazi wao kulazimika kwenda mbali kwa ajili ya huduma hizo.

Aidha,amewataka wananchi wa kata hiyo kupenda kushiriki na kuchangia nguvu zao katika shughuli mbalimbali za maendeleo,badala ya kuichia serikali peke yake kwani kufanya hivyo itasaidia miradi inayoibuliwa na kutekelezwa kukamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Mbinga Grace Quintine amesema,kwa mwaka wa fedha 2022/2023 wamepokea kiasi cha shilingi milioni  150 kutoka serikali kuu zilizotumika kujenga zahanati tatu ikiwamo ya kata ya Matarawe ambayo ujenzi wako uko hatua ya mwisho kukamilika.

Quintine amesema,zahanati hiyo na nyingine zitakapomilika zitasaidia kutatua changamoto ya wananchi wa maeneo husika kutembea umbali mrefu na kutumia muda mwingi kwenda maeneo mengine kufuata huduma za  afya.

Aidha amesema, Halmashauri ya Mji Mbinga kutoka mapato ya ndani imetenga na kutumia shilingi milioni  89 zilizofanikisha kujenga zahanati mbili ambazo zimekamilika  na kuanza kutoa huduma za afya kwa wananchi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.