• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Mbinga wakamilisha ujenzi wa zahanati,waomba ifunguliwe

Imewekwa kuanzia tarehe: February 15th, 2023

BAADHI ya wananchi wa kata ya Luwaita Halmashauri ya mji Mbinga wilayani Mbinga,wameiomba serikali kupitia Halmashauri ya Mji Mbinga,kukamilisha  ujenzi wa zahanati ya Luwaita kutokana na ujenzi wake kuchukua zaidi ya miaka 5 bila kukamilika.

Wamesema kukosekana kwa huduma za afya katika kata hiyo,kumesababisha  akina mama wajawazito kulazimika kujifungulia njiani kutokana na vituo vya afya vilivyopo kuwa umbali wa zaidi ya kilomita 7 kutoka katika maeneo wanayoishi.

Wameiomba Halmashauri ya mji Mbinga ,kuwahurumia kutokana na mateso wanayopata kutumia muda mwingi kwenda kupata huduma maeneo mengine kwa kuanza mchakato wa kufungua na kutoa  baadhi ya huduma katika zahanati hiyo ambayo sehemu kubwa ujenzi wake umekamilika.

Bosco Komba amesema, zahanati hiyo ilianza kujengwa kwa muda mrefu kwa wananchi kuchangia nguvu zao ili waweze kupata huduma za matibabu karibu,hata hivyo wanashangazwa na ukimya wa serikali kushindwa kufungua na kutoa huduma kwa wananchi.


Maria Nchimbi amesema,wananchi wa  kata ya Luwaita wanatamani kuona zahanati hiyo ikianza kutoa huduma kwani wamechoka kuvumilia kutembea umbali mrefu kila wanapohitji kupata huduma za matibabu ambazo zinapatikana kwenye vituo vilivyopo mbali na makazi yao.

Mtendaji wa kijiji cha Luwaita Rehema Ameir ameeleza kuwa,awali mpango wa serikali ulikuwa kituo cha afya,lakini kukosekana kwa nguvu kazi za wananchi ikaamua iwe zahanati kwa kuwa zilihitajika nguvu za pamoja kati ya serikali na wananchi wa eneo husika.

Hata hivyo amesema,ujenzi wa zahanati ya Luwaita umekamilika kwa asilimia 99 na wakazi zaidi ya 4,000 wanatarajia kupata huduma mara itakapoanza kutoa huduma,lakini kuchelewa kufunguliwa kunatokana na kukosekana kwa vyoo na kichomea taka.

Amesema,zahanati hiyo itarahisisha upatikanaji wa huduma na kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kwenda kutafuta  huduma kwenye vituo vingine vya afya  na kupunguza muda mwingi wanaopaswa kujikita katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa Halmashauri ya mji Mbinga Dkt Maximo Magehema amesema,kimsingi zahanati hiyo imekamilika na serikali ipo katika hatua ya mwisho kuanza kutoa huduma na kuwaomba wananchi kuwa wavumilivu wakati serikali ikikamilisha mambo muhimu ya kiutendaji ikiwamo vifaa na watumishi.

Amesema,serikali ya awamu ya sita kupitia Halmashauri ya mji Mbinga imejipanga kuhakikisha kila kijiji kina zahanati na kata  kituo cha afya ili kusogeza na kuboresha  huduma za afya kwa wananchi wake.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.