• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Mbinga watakiwa kuchangamkia fursa ya punguzo ya umilikishwaji ardhi

Imewekwa kuanzia tarehe: October 29th, 2023

 Maafisa Ardhi wa Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wamewataka wananchi kuchangamkia fursa ya punguzo la asilimia 42.9 ya bei ya umilikishwaji wa ardhi baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa ofa hiyo.

 Afisa Ardhi Mteule wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga France Kaganda, alieleza kuwa  kuanzia Julai Mosi, 2023, gharama zimepungua kutoka Shilingi 163,000  hadi Shilingi 93,000 kwa kiwanja chenye mita za mraba 600.

Bw. Kaganda alikuwa anazungumza  wakati  kwenye kilele cha kampeni maalum ya siku nne ya kutoa elimu ya masuala yahusuyo usimamizi wa sheria, kanuni na taratibu za uendelezaji wa ardhi, kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi katika Wilaya ya Mbinga.  

"Tunawataka  wananchi wote wenye viwanja ambavyo vimepimwa na vina sifa ya kuandaliwa hati kujitokeza ili kupata nyaraka za hati miliki," alisema  Bw. Kaganda.

Aliongeza kuwa mwananchi akilipa kodi ya ardhi na kupeleka vithibitisho vyote katika idara ya Ardhi, ataandaliwa na kupatiwa hati yake ndani ya siku 14.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo aliwataka maafisa Ardhi kutoa hati miliki kwa wakati ili watu waanze shughuli za ujenzi kwa wale wanaohitaji kujenga.

Aliwaasa wananchi kufuata ushauri wa wataalamu wa ardhi ili kuepuka athari mbalimbali zinazoweza kujitokeza baadae ikiwa ni pamoja na kubomolewa nyumba au kupitiwa na mafuriko.

"Watu wengi wamekuwa wakipigana na kuumizana kutokana na migogoro ya ardhi, ninakiagiza kitengo cha Ardhi kuwa wasuluhishi zaidi kuliko kuwa chanzo cha migogoro," aliagiza Mhe. Aziza

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Bi. Amina Seif alisema kuwaona wataalamu wa ardhi na kupata hati miliki pamoja na ushauri itasaidia kupunguza au kuondoa migogoro ya ardhi.  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.