• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Ruvuma waaswa kuacha kusafisha mashamba kwa kutumia moto

Imewekwa kuanzia tarehe: October 11th, 2024

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),umewataka wananchi hususani wanaojishughulisha na kilimo kuacha kutumia moto kama njia ya kusafisha mashamba yao.
Badala yake wameshauriwa kutumia mbinu mbadala ikiwemo majembe na zana nyingine ili kuepusha uharibifu wa mazingira unaoweza kusababisha majanga ya moto katika misitu na uoto wa asili.


Wito huo umetolewa na Mhifadhi Misitu Mwandamizi wa TFS John Kimolo, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari waliotembelea shamba la miti Mpepo kata ya Mpepo wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.
Amesema,wakulima wanapotaka kuandaa na kusafisha mashamba yao wanapaswa kuchukua tahadhari na kupata ushauri wa kitaalamu ili kuepuka kutokea kwa majanga ya moto katika misitu ya asili na miti ya kupandwa na maeneo ya uoto wa asili.

“wananchi wanapoandaa mashamba yao wanatakiwa kufyeka nyasi na miti na kukusanya mabiwi na wachome kwa kuzingatia mwelekeo wa upepo,sisi kama shamba la miti Mpepo tutaendelea kutoa elimu juu ya kuzingatia utumiaji sahihi wa moto kwenye mashamba”alisema Kimolo.


Amesema,Shamba la miti Mpepo limeanzisha bustani ya miti ambayo inapandwa kwenye mashamba ya Serikali,taasisi za Serikali na kugawa miche ya miti kwa watu binafsi ili waweze kupande katika maeneo yao kwa ajili ya kujiongezea kipato.

Kwa mujibu wa Kimolo,katika bustani hiyo miche ya miti inayooteshwa ni jamii ya misindano inayopandwa mahususi kwenye mashamba yaliyopo safu za Mpepo,Kivulungwa na Lusewa ambazo zinastawi vizuri miti.

Amesema,safu na Liuli zilizopo pembezoni mwa ziwa Nyasa imepandwa miti ya aina ya misaji(tiki)inayostawi vizuri kwenye ukanda wa chini.

Diwani wa Kata ya Mpepo Mheshimiwa Anderson Haule amesema,tangu Serikali kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ilipoanzisha mradi wa upandaji miti umesaidia wananchi wa kata hiyo kupata ajira za muda na wengine ajira za kudumu na hivyo kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana na wanawake.









Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.