• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Ruvuma wanufaika na huduma ya ujazilizi umeme

Imewekwa kuanzia tarehe: February 23rd, 2025

Wananchi wa mitaa ya Namakinga na Dodoma, katika Kata ya Maposeni na Peramiho, mkoani Ruvuma, wamepokea kwa shukrani mradi wa ujazilizi wa umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Wakazi wa maeneo hayo wamesema mradi huu utaboresha maisha yao kwa kuwawezesha kupata huduma za kijamii na fursa za kiuchumi.

Afisa Habari na Uhusiano wa TANESCO mkoani Ruvuma, Allan Njiro, amewatembelea wananchi hao na kuwapa elimu kuhusu taratibu za kupata huduma ya umeme. Ameeleza kuwa wananchi wanaounganishiwa umeme kwa matumizi ya nyumbani wanapaswa kulipa shilingi 27,000, huku wale wa matumizi ya viwanda wakilipa shilingi 139,000.

Aidha, Njiro amefafanua kuwa ili kuunganishiwa umeme, wananchi wanapaswa kufanya maombi kwa njia ya simu, kuwa na kitambulisho cha NIDA, kuhakikisha nyumba zao zimefanyiwa wiring na mkandarasi, na kuhakiki uwepo wa nguzo za umeme. Amesisitiza kuwa ada ya kuunganishiwa umeme inabaki kuwa bure, huku gharama za vifaa vya ndani zikibebwa na wananchi wenyewe.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Habari wa Huduma kwa Wateja, Emma Ulendo, amewahimiza wananchi kutumia fursa hii kwa manufaa ya jamii. Amesema kuwa gharama za kuunganishiwa umeme kwa wananchi wa Songea Vijijini ni shilingi 27,000, huku wale wa mijini wakitakiwa kulipa shilingi 321,000. Amehimiza wakazi kuhakikisha nyumba zao zinafanyiwa wiring kwa viwango sahihi ili kuepuka hatari za umeme.

Diwani wa Kata ya Maposeni, Monica Tambara, ameipongeza TANESCO kwa kutoa elimu kuhusu utunzaji wa miundombinu ya umeme. Pia, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuhakikisha wananchi wanapata umeme kwa gharama nafuu na kumpongeza Mbunge wa Songea Vijijini, Jenista Mhagama, kwa kuendeleza maendeleo ya eneo hilo.

Serikali imeendelea kusisitiza ushirikiano wa wananchi katika kuutunza mradi huu wa REA ili kuhakikisha unawanufaisha kwa muda mrefu. Mradi huu unatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta za biashara, elimu na afya, hivyo kuchochea maendeleo kwa wananchi wa Namakinga na Dodoma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.