• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Ruvuma waongezeka kwa asilimia 2.9

Imewekwa kuanzia tarehe: June 21st, 2023

IDADI ya watu katika mkoa wa Ruvuma imeongezeka kutoka watu milioni 1,376,891 mwaka 2012,hadi kufikia    1,848,794 sawa na ongezeko la watu 471,903 katika kipindi cha miaka kumi.

Idadi hiyo inaonyesha kiwango cha ukuaji wa watu katika mkoa huo kimeongezeka kutoka asilimia 2.1 hadi asilimia 2.9 ikiwa ni chini ya kiwango cha kasi ya ongezeko la idadi ya watu kitaifa ambayo ni asilimia 3.2 kwa mwaka 2022.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa hu Kanal Laban Thomas,wakati akifungua semina ya uwasilishaji,usambazaji na uhamasishaji matumizi ya matokeo ya Sensa kwa viongozi na watendaji wa  mkoa wa Ruvuma iliyofanyika katika ukumbi wa Parokia ya Bombambili mjini Songea.

Alisema kutokana na kasi kubwa ya ongezeko la watu,viongozi wa mkoa huo wanapaswa kujipanga vyema na kuweka mikakati madhubuti na endelevu  kwa kutoa huduma bora za kijamii na za kiuchumi kwa wananchi ili kuimarisha ustawi wao na maendeleo ya mkoa  huo.

Kanal Laban,amewataka viongozi na watendaji kuhakikisha kuwa mipango yao ya maendeleo ya muda mfupi,muda wa kati na muda mrefu yanazingatia idadi ya watu,mahitaji yao na  mazingira wanayoishi inazingatia matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Ametaka mipango hiyo izingatie mwenendo wa ongezeko la kasi ya ukuaji wa idadi ya watu ili mkoa huo unakuwa miongoni mwa mikoa ya mfano katika matumizi ya takwimu zilizotolewa na Ofisi ya taifa ya Takwimu nchini.

Aidha amewaasa viongozi na watendaji  katika ngazi zote za kiutawala katika mkoa huo,kuhakikisha wanasimamia vyema maendeleo  na kugawa rasilimali za taifa kwa kufuata vigezo vya kitakwimu,badala ya kugawa kwa upendeleo.

Ametaka,matumizi mazuri ya matokeo ya sensa katika kufanya maamuzi yenye kufuata vigezo vya kitakwimu na kuepuka kufuata au kutekeleza matakwa binafsi au maagizo ya baadhi ya watu binfasi.

Kanal Laban,amewapongeza na kuwashukuru viongozi na watendaji kuanzia ngazi ya mkoa,mitaa,vitongoji na wananchi wa mkoa huo kwa ushirikiano na mshikamano walionesha wakati wa mchakato mzima wa maandalizi ya sensa hadi kukamilika tarehe 5 Septemba 2022.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania Dkt Albina Chuwa, Mratibu wa Sensa ya watu na makazi mkoa wa Ruvuma Mwamtumu Athuman alisema,semina hiyo inalenga kuongeza uwezo wa kuwafahamisha na kuwaelimisha wananchi namna ya kupata matokeo ya sensa na kuyatumia katika shughuli zao binafsi za kuinua hali zao za maisha

Alisema,uelewa mzuri wa wananchi wa matumizi ya matokeo ya sensa utasaidia sana kutoa mchango wao katika maendeleo ya Taifa kwa kushiriki vyema,kufanya maamuzi na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za maendeleo zinazofanywa na Serikali na wadau wengine wa maendeleo.

Pia alisema,hatua hiyo itasaidia kuongeza uwajibikaji kwa  watendaji na viongozi wa kuchaguliwa wakiwemo Wabunge  na madiwani ambao wanapaswa kuyaelewa na kuyatumia  matokeo  ya sensa ya mwaka 2022 kama dira katika kufanya maamuzi yanayohusu maendeleo  ya wananchi.

Athuman,ameipongeza wilaya ya Tunduru kwa kufanya vizuri katika  sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 na kuwaomba wadau wote kupeleka maombi au maoni ofisi ya Taifa ya Takwimu kuhusiana na matokeo ya zoezi la sensa  ya watu na makazi ili yaweze kufanyiwa kazi.

Naye Mratibu wa Sensa Taifa Seif Kuchengo alisema,katika mkoa wa Ruvuma wilaya inayoongoza kuwa na idadi kubwa ya watu ni  Tunduru yenye jumla ya watu laki 4.12 ikifuatiwa na Manispaa ya Songea yenye watu laki 2.86 na Halmashauri ya mwisho Madaba yenye wakazi elfu 65,215.

Aliongeza kuwa,idadi hiyo inaifanya Halmashauri ya wilaya Tunduru kuwa na zaidi ya asilimia 23.6 ya watu wote wa mkoa wa Ruvuma na Halmashauri ya Madaba kuwa na asilimia 3 tu ya wakazi wote wa mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.