• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Ruvuma washauriwa kutoa maoni ya Dira mpya ya Maendeleo 2050

Imewekwa kuanzia tarehe: January 29th, 2024

Na Albano Midelo,Songea

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ametoa rai kwa  wananchi kushiriki kikamilifu kutoa  maoni katika maandalizi ya Dira mpya ya maendeleo ya 2050.

Kanali Thomas ametoa rai hiyo wakati  anafungua mafunzo ya matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa viongozi na watendaji wa Mkoa,Kamati ya Sensa ya Mkoa,wadau na makundi maalum katika jamii yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Parokia ya Bombambili mjini Songea.

Amesema Dira ya maendeleo ya 2025 inaelekea ukingoni ambapo serikali inaandaa Dira mpya ya 2050 ambapo ameshauri kutumia matokeo ya Sensa ya 2022 na t takwimu nyingine katika kutoa maoni na mapendekezo.

“Hatuna budi kutoa maoni yetu kwa Tanzania tunayoitarajia ifikapo mwaka 2050,tuna bahati serikali yetu imetuwekea njia mbalimbali za kutuwezesha kutoa maoni na mapendekezo yetu’’,alisisitiza RC Thomas.

Akizungumzia mafunzo hayo,Mkuu wa Mkoa amesema semina hiyo ni mfululizo wa mafunzo ya usambazaji na uhamasishaji wa matumizi ya matokeo ya sensa ya mwaka 2022  kama ilivyoelekezwa kwenye Mwongozo wa kitaifa wa matumizi ya matokeo ya sensa uliozinduliwa Oktoba 2022 na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati anazindua matokeo ya mwanzo ya sensa.

Mkuu wa Mkoa ameipongeza serikali ya Awamu ya Sita kwa kuandaa Mwongozo huo ambao unaimarisha uwezo wa viongozi na wananchi katika kupanga,kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa mipango na program za maendeleo.

Ameyataja mafunzo hayo kuwa yana umuhimu wa kipekee kwa washiriki kwa sababu yatawawezesha kutekeleza majukumu ya uongozi na utendaji kwa umakini,weledi,na usahihi zaidi hivyo kuharakisha maendeleo ya Mkoa.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mwantumu Athuman ameyataja malengo ya mafunzo hayo kuwa ni kuwajengea wadau uwezo wa kutafsiri,kuchambua na kuyatumia matokeo ya Sensa katika kupanga,kutekeleza,kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera,mipango na program mbalimbali za maendeleo.

Amesisitiza kuwa utekelezaji wa Sensa ya watu na makazi ni uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali ili kupata taarifa muhimu na za msingi kuhusu watu wake, kidemografia ,kiuchumi na kimazingira.

Hata hivyo ameyataja madhumuni ya kupata taarifa hizo ni kuzitumia kwa kuhuisha sera,kupanga mipango na program za maendeleo na kufuatilia utekelezaji wake.

Ameitaja moja ya faida kubwa ya matumizi sahihi ya matokeo ya Sensa ni kuongeza ufanisi katika matumizi ya rasilimali za nchi kwa kufanya maamuzi yanayohusu maendeleo ya nchi kwa kuzingatia idadi ya watu,mahitaji yao na mazingira wanamoishi.

Kaulimbiu ya awamu ya tatu ya utekelezaji wa sensa ni Matokeo ya Sensa ya Sita,Mipango Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.